MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kituo Cha Kubadilishia Njia Za Usambazaji Umeme Chazinduliwa Kongwa,Dodoma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kituo Cha Kubadilishia Njia Za Usambazaji Umeme Chazinduliwa Kongwa,Dodoma
Habari

Kituo Cha Kubadilishia Njia Za Usambazaji Umeme Chazinduliwa Kongwa,Dodoma

Author
By Author
Share
5 Min Read
Na Lucy Lyatuu,Dodoma
SERIKALI imezindua kituo cha Kubadilishia Njia za Usambazaji Umeme (Switching Station) pamoja na Transforma ya Kudhibiti Umeme (AVR)  ikiwa ni sehemu muhimu ya jitihada za za kuimarisha uthabiti wa mfumo wa usambazaji wa umeme na kuongeza uhakika wa huduma kwa wananchi.
Akizindua kituo hicho mkoani hapa katika wilaya ya Kongwa , WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema kupitia uwekezaji wa Serikali wa zaidi ya sh bilioni 10.5,  Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imefanikiwa kujenga Kituo cha Kubadilishia Njia za Usambazaji Umeme.
Amesema  ujenzi huo pia umehusisha  kusimika Transforma ya Kudhibiti Umeme yenye uwezo wa MVA 20 pamoja na miundombinu mingine ikiwemo njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Zuzu hadi Mbande yenye urefu wa kilomita 92.
Habari Picha 12370
Ndejembi amesema Serikali imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini.
Aidha amesema Serikali inaendelea na mipango mbalimbali ya kuongeza uwezo huo ili kufikia zaidi ya megawati 8,000 katika miaka ijayo  pamoja na mahitaji ya maendeleo ya Taifa na matarajio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050.
 Amesema kutokana na umuhimu huo, Serikali imeendelea kuupa Mkoa huo kipaumbele maalum katika uwekezaji wa miundombinu ya nishati ili kuhakikisha huduma ya umeme inakuwa ya uhakika, salama na yenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya taasisi za Serikali, sekta binafsi, wawekezaji na wananchi kwa ujumla.
Habari Picha 12371
“Kwa kutambua ukuaji wa haraka wa Mkoa wa Dodoma na ongezeko la mahitaji ya huduma ya umeme, Wizara ya Nishati kupitia TANESCO imeendelea kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kuimarisha usafirishaji na usambazaji wa umeme mkoani hapa,” amesema.
Amesema lengo ni kuona Mkoa wa Dodoma unaendelea kuwa mfano wa upatikanaji wa huduma bora za umeme zinazowezesha utoaji wa huduma za Serikali, ukuaji wa biashara, uwekezaji wa viwanda na maendeleo ya kijamii yanayostahili Makao Makuu ya Taifa.
Amesema ni katika muktadha huo ndipo Serikali ilipoidhinisha utekelezaji wa mradi tunaouzindua leo hapa Mbande.
Amesema Kwa muda mrefu, wananchi wa Wilaya ya Kongwa walitegemea njia moja ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Dodoma Mjini, hali iliyokuwa ikisababisha changamoto za upatikanaji wa umeme wa uhakika kutokana na ongezeko la mahitaji ya huduma hiyo.
Amesema  Kukamilika kwa miundombinu hii kutaimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme katika Wilaya za Kongwa, Gairo, Chamwino pamoja na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Mpwapwa.
Habari Picha 12372
Kwa wananchi wa Kongwa na maeneo yote yanayonufaika na mradi huu, ninawahimiza kuendelea kuitunza miundombinu hii na kutumia fursa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika kuongeza uzalishaji, kukuza biashara na kuboresha maisha yao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Wa TANESCO,Lazaro Twange amesema uzinduzi huo   ni muhimu kwa wananchi wa Wilaya za Kongwa, Chamwino,Gairo,na baadhi ya maeneo ya Mpwapwa katika Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.
Amesema hayo ni matokeo ya uwekezaji wa Serikali katika kuimarisha miundombinu ya usambazaji wa umeme na kuongeza uhakika wa huduma kwa wananchi.
Amesema Shirika limeendelea kufanya tathmini ya mahitaji ya huduma ya umeme katika maeneo mbalimbali nchini na kuandaa miradi ya kimkakati inayolenga kuimarisha mfumo wa usafirishaji na usambazaji wa umeme.
“Kupitia tathmini hizo, ilibainika kuwa pamoja na ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii katika Wilaya ya Kongwa na maeneo jirani, kulikuwa na haja ya kuimarisha uthabiti wa mfumo wa usambazaji wa umeme ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya huduma hiyo.,” amesema.
Amesema Kwa muda mrefu, wananchi wa Kongwa walitegemea njia moja ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Dodoma Mjini, hali iliyokuwa ikisababisha changamoto za upatikanaji wa umeme wa uhakika hususan wakati wa matengenezo au hitilafu za kiufundi.
Habari Picha 12373
Amesema Kutokana na hali hiyo, TANESCO iliona umuhimu wa kuwekeza katika miundombinu itakayoongeza uwezo wa mfumo wa usambazaji wa umeme, kuboresha viwango vya huduma na kuweka mazingira bora ya maendeleo kwa wananchi wa Kongwa na maeneo jirani.
Amesemaiundombinu hiyo itatoa  uthabiti wa mfumo wa usambazaji wa umeme, kupunguza athari za hitilafu, kuboresha viwango vya umeme na kuongeza uwezo wa TANESCO kuhudumia wateja waliopo pamoja na mahitaji yatakayojitokeza katika siku zijazo.

You Might Also Like

Dirisha  La Udahili Awamu Ya Pili Lafunguliwa-TCU

Serikali kuleta kicheko kwa TASU 

Sweden na UNFPA Kuwawezesha Vijana na Akina Mama Kituo cha Ufundi cha Yombo

CCCC Yaandaa Tamasha La Dragon Boat

Mtasingwa Aitaka Serikali Kuwatengea Eneo Wafanyabiashara wa Senene Bukoba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kiswahili Chavuka Mipaka, Paris Yajiandaa Kukipokea
Next Article Mhitimu Mwenye Ulemavu Aivutia Serikali kwa Ubunifu wa Ramani VETA
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Jua Namba Zako Okoa Maisha Yako
Habari June 19, 2026
Hananja Awataka Vijana Kufikiri Mara Mbili Kabla ya Kufuata Wito wa Maandamano
Habari June 18, 2026
June 18, 2026
Habari June 18, 2026
Magereza Yaomba Jamii Kuwapokea Wafungwa Wanaorejea Kutumikia Taifa
Habari June 18, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?