MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wizara Ya Nishati Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050,Kuhamasisha Matumizi Ya  Nishati Safi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wizara Ya Nishati Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050,Kuhamasisha Matumizi Ya  Nishati Safi
Habari

Wizara Ya Nishati Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050,Kuhamasisha Matumizi Ya  Nishati Safi

Author
By Author
Share
2 Min Read

 


Na Lucy Lyatuu,Dodoma

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi asilia, Dkt. James Mataragio, ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kama sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2050 inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ambayo ni salama na endelevu.

Dkt. Mataragio ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la Shirika La Umeme (TANESCO) eneo la nishati safi ya kupikia kwa umeme , katika maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma.

Habari Picha 11846

Amesema kuwa Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ikiwa ni pamoja na umeme, ili kulinda afya za wananchi na mazingira kwa ujumla, Aidha, ameipongeza TANESCO kwa juhudi zake za kuelimisha na kuhamasisha wananchi kutumia umeme kupikia.

‘’ Bajeti ya Nishati inatarajiwa kusomwa Bungeni, miongoni mwa mambo tunayotekeleza katika Bajeti yetu ni Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ,hapo kuna kipengele cha nishati safi ya kupikia na kwa ujumla Taasisi zetu ikiwemo TANESCO zinahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupika kwa umeme,’’amefafanua Dkt Mataragio.

Kwa upande wake, Mbunge kutoka Manyara, M Justina Rahhi, amesifu teknolojia ya majiko ya umeme yanayotumia nishati kidogo, akieleza kuwa yana uwezo wa kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.

Habari Picha 11847

“Nimejifunza kuwa majiko haya yanatumia umeme kidogo sana ukilinganisha na mkaa. Ni muhimu teknolojia hii iwafikie wananchi wa vijijini ili waweze kunufaika na matumizi ya nishati safi,” amesema Rahhi

Naye Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Ruvuma, Mariam Nyoka, amepongeza kuimarika kwa huduma ya umeme katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, akieleza kuwa hali hiyo itasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi.

Katika maonesho hayo ya Wiki ya Nishati, TANESCO pia imewasilisha teknolojia mpya ya magari yanayotumia umeme, ambayo yanaelezwa kuwa na gharama nafuu zaidi kwa matumizi ikilinganishwa na magari yanayotumia nishati nyingine.

You Might Also Like

Tanzania Kuwa Mwenyeji Wa Mkutano Wa Petroli Afrika

Ruto: Diplomasia Itumike Kumaliza Mgogoro Kongo

Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini

Serikali Yazidi Kuhamasisha Nishati Safi, Yatoa Mitungi 225 Kwa Watumishi Gereza kuu Maweni

TARURA Yaimarisha Upitikaji Miundombinu Ya Barabara

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mandingo: Jiungeni Mkunga Marathon Kuokoa Maisha ya Mama na Mtoto
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mandingo: Jiungeni Mkunga Marathon Kuokoa Maisha ya Mama na Mtoto
Habari April 21, 2026
‘Upungufu wa Wakunga Afrika Watishia Maisha ya Mama na Mtoto ‘TAMA
Habari April 21, 2026
Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?