MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Habari

Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MOROGORO: WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ameridhishwa na utekelezaji wa miradi 81 ya dharura iliyosimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), akieleza kuwa imekamilika kwa wakati na kwa viwango vya juu vya ubora.
Akifungua Mkutano wa 21 wa Baraza la Wafanyakazi wa TANROADS mkoani Morogoro, Ulega amesema mafanikio hayo yanadhihirisha kukua kwa uwezo wa makandarasi wazawa na wataalamu wa ndani.
Amefafanua kuwa miradi hiyo, iliyohusisha ujenzi wa madaraja na makalvati kupitia mpango wa CERC, imekuwa msaada mkubwa katika kupunguza athari za mvua na mafuriko.
Ameishukuru Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha, akisema uwekezaji huo umeanza kuleta matokeo chanya, ikiwemo kupungua kwa uharibifu wa miundombinu licha ya mvua zinazoendelea kunyesha mwaka huu.
Ulega amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya maeneo yenye uhitaji wa madaraja ya kisasa, huku akiwataka watumishi wa TANROADS kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ubunifu.
Pia ameelekeza matengenezo ya barabara na madaraja yafanyike kwa wakati ili kupunguza usumbufu kwa wananchi.
Aidha, amesisitiza utekelezaji wa mpango wa kupendezesha barabara kwa kupanda miti ya kivuli na matunda pamoja na kuimarisha taa za barabarani.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mussa Kilakala, ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za awali kwa ujenzi wa barabara ya Bigwa–Kisaki, akibainisha kuwa wananchi watanufaika na mradi huo.
Naye Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mohamed Besta, amesema mkutano huo unalenga kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika maamuzi, huku Menejimenti ikiahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yote kwa ufanisi.

You Might Also Like

Bunge Bonanza 2026 Kuikutanisha Simba Na Yanga Dodoma

Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima

DKT. Biteko Azindua Mradi Utakaowakwamua Vijana Kiuchumi Katika Maeneo Yanayopitiwa Na Bomba La Mafuta Ghafi  (EACOP)

Ridhiwan Kikwete Apongeza Halmashauri Ya Tunduma

Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji
Next Article Ubunifu Wa Majengo Watakiwa Kuzingatia Tija Na Gharama Nafuu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Utafiti wa Chakula Bora cha Kuku wa Nyama Watoa Tumaini kwa Wafugaji
Makala May 19, 2026
JWTZ Kulipa Fidia Wananchi Waliochukuliwa Maeneo
Habari May 19, 2026
Timu Ya Bunge Yakabidhiwa Vifaa Vya Michezo
Habari May 19, 2026
Ndoinyo Aishauri Serikali Kurejesha Utalii Vijijini
Habari May 19, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?