MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ziwa Victoria Lanufaisha Watu Milioni 45 Afrika Mashariki – Mtanda
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ziwa Victoria Lanufaisha Watu Milioni 45 Afrika Mashariki – Mtanda
Habari

Ziwa Victoria Lanufaisha Watu Milioni 45 Afrika Mashariki – Mtanda

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Lucy Ngowi, Mwanza
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amesema zaidi ya watu milioni 45 wanaoishi katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wananufaika na uwepo wa Ziwa Victoria, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha rasilimali hiyo muhimu inalindwa na kutunzwa kwa mipango endelevu.
Mtanda amesema hayo wakati wa uzinduzi wa maonesho yanayoambatana na maadhimisho ya Siku ya Ziwa Victoria, ambayo kilele chake kitafanyika Alhamisi, Mei 21, 2026 jijini Mwanza.
Amesema Siku ya Ziwa Victoria ilianzishwa baada ya mawaziri wa sekta za Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na wakuu wa nchi wanachama kukubaliana kuwa na maadhimisho hayo kila mwaka ifikapo Mei 21 kwa lengo la kuhamasisha uhifadhi na matumizi endelevu ya ziwa hilo.
Amesema, kwa mara ya kwanza maadhimisho hayo yanafanyika Mwanza, nchini Tanzania, jambo ambalo amesema ni heshima kubwa kwa nchi.
Ameshukuru Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa kwanza wa maadhimisho hayo muhimu.
Mtanda amesema Ziwa Victoria ni rasilimali kubwa ambayo Mungu ameijalia Afrika Mashariki, huku Tanzania ikimiliki asilimia 51 ya eneo lote la ziwa hilo, Uganda asilimia 43 na Kenya asilimia sita.
Ameongeza kuwa Bonde la Ziwa Victoria linaenea hadi Burundi na Rwanda, likiwezesha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Ametaja shughuli zinazonufaika na ziwa hilo kuwa ni pamoja na kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii, uhifadhi wa wanyamapori pamoja na usafirishaji.
Aidha, amesema Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki imeleta mradi mkubwa wa uokozi wenye thamani ya zaidi ya Sh Bilioni tano, ukiwa na boti na vifaa vya kisasa vya uokoaji ili kuongeza usalama ndani ya ziwa.
Akizungumzia kauli mbiu ya mwaka huu ya “Maji Yetu, Mustakabali Wetu tuungane kwa usimamizi endelevu wa Bonde la Ziwa Victoria,” Mtanda amesema mustakabali wa maisha ya binadamu na maendeleo ya kiuchumi na kijamii unategemea upatikanaji wa maji, hivyo kuna umuhimu wa kuunganisha nguvu katika kulinda na kuhifadhi Ziwa Victoria.
Amesema wananchi wa Mwanza wameanza kuchukua hatua za kuhifadhi vyanzo vya maji ikiwemo eneo la Butimba, huku serikali ikiendelea kudhibiti changamoto ya gugu maji ambayo iliwahi kuathiri shughuli za kiuchumi ndani ya ziwa hilo.
Mtanda ameongeza kuwa uchumi wa vizimba vya samaki unaendelea kukua mkoani Mwanza, lakini akasisitiza kuwa uchafuzi wa ziwa unaweza kuathiri uzalishaji huo pamoja na upatikanaji wa maji ya kutosha kwa wananchi.
Katika kilele cha maadhimisho hayo, wageni mbalimbali kutoka mikoa ya ukanda wa Ziwa Victoria wanatarajiwa kushiriki katika shughuli hiyo muhimu.

You Might Also Like

Mifugo Mingi Chanzo Cha Uchafuzi Maji Ziwa Victoria

Madini Yaweka Rekodi Makusanyo Ya Maduhuli

Mkurugenzi Mkuu Wa NSSF Aongoza Utoaji Wa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii Soko La Tegeta Nyuki

Kusiluka aitaka TVLA kuongeza tafiti za chanjo 

Nchemba Afungua Mafunzo Ya PAC

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Ataka Vijiji Vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro Kulipwa Fedha Za Uwajibikaji
Next Article Inzi Chuma: Suluhisho la Chakula cha Mifugo, Uhifadhi wa Mazingira
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nyavu za Plastiki Zatishia Afya za Watumiaji wa Samaki Ziwa Victoria
Habari May 19, 2026
Utunzaji Ziwa Victoria Wasisitizwa kwa Mustakabali wa Uchumi, Mazingira
Habari May 19, 2026
Inzi Chuma: Suluhisho la Chakula cha Mifugo, Uhifadhi wa Mazingira
Makala May 18, 2026
Mbunge Ataka Vijiji Vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro Kulipwa Fedha Za Uwajibikaji
Habari May 18, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?