MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TPHPA Yasisitiza Matumizi Sahihi ya Viuatilifu kwa Wakulima
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TPHPA Yasisitiza Matumizi Sahihi ya Viuatilifu kwa Wakulima
Habari

TPHPA Yasisitiza Matumizi Sahihi ya Viuatilifu kwa Wakulima

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imeendelea kuhamasisha matumizi sahihi ya viuatilifu kwa wakulima na wafanyabiashara, ikieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuongeza uzalishaji wa mazao na kulinda afya ya binadamu pamoja na mazingira.
Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkaguzi wa Biashara ya Viuatilifu wa TPHPA, Ereneus Mwinuka, amesema wakulima wengi bado wanakabiliwa na changamoto ya kutotambua viuatilifu vinavyofaa kwa ajili ya kudhibiti wadudu na magonjwa yanayoshambulia mazao yao.
Amesema mamlaka hiyo inatumia maonesho hayo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kusoma taarifa zilizopo kwenye lebo za viuatilifu kabla ya matumizi, ili kuhakikisha wanachagua bidhaa sahihi kulingana na aina ya kisumbufu wanachotaka kudhibiti.
Kwa mujibu wa Mwinuka, matumizi ya viuatilifu visivyofaa yanaweza kusababisha hasara kwa mkulima kutokana na kushindwa kudhibiti tatizo husika, hivyo ni muhimu kutambua kwanza kisumbufu kabla ya kufanya ununuzi wa bidhaa.
Aidha, amewataka wakulima kuhakikisha wanatumia viuatilifu vilivyosajiliwa na kuthibitishwa na TPHPA kwa kuangalia namba za usajili pamoja na tarehe ya mwisho wa matumizi ili kuepuka matumizi ya bidhaa zisizo salama au zisizo na ufanisi.
Mbali na wakulima, TPHPA pia imekuwa ikitoa elimu kwa wafanyabiashara wa viuatilifu kuhusu taratibu za biashara hiyo, ikiwemo masharti ya kupata leseni na wajibu wao wa kuwapa wakulima ushauri sahihi kuhusu matumizi ya bidhaa wanazouza.
Mwinuka amesema mwitikio wa wananchi kutembelea banda la mamlaka hiyo umekuwa mkubwa, jambo linaloonyesha kuongezeka kwa uelewa na hamasa ya kutafuta taarifa sahihi kuhusu matumizi ya viuatilifu.
Ameeleza kuwa wageni wengi waliotembelea banda hilo wamepata maarifa mapya yatakayowasaidia kufanya maamuzi bora wakati wa kununua na kutumia viuatilifu katika shughuli za kilimo.

You Might Also Like

Wanafunzi 571 watunukiwa Stashahada Na Astashaha Za Vyuo Vya Polisi

Kamishna TFS Aongoza Kikao Cha Viongozi Wa Kamisheni ya Misitu Afrika

Atoa Maelekezo Kwa Chuo Cha Hombolo Kuwajengea Uwezo Viongozi Wa Mitaa Na Vijiji -Kapinga

Ridhiwani, Waziri Wa Kazi, Ajira UAE Waweka mkakati

Ndizi, Mchele, Mafuta Vyapanda Bei

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article BRELA Yahamasisha Urasimishaji wa Biashara kwa Ukuaji wa Uchumi
Next Article Magereza Yaomba Jamii Kuwapokea Wafungwa Wanaorejea Kutumikia Taifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mfumo Wa Kidijitali Wa PSSSF Wamvutia Mkurugenzi Wa BOT
Habari August 5, 2026
FAO Yasisitiza Kutowapa Mifugo Dawa Bila Maelekezo Ya Watalaam
Habari August 5, 2026
Balozi Wa Kudumu Wa Mashirika Ya UN Atembelea FAO Nanenane
Habari August 5, 2026
Wadau Wamiminika Banda La REA Katika Maonesho Ya Nanenane  2026
Habari August 5, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?