Na Mwandishi Wetu
WADAU mbalimbali wameendelea kufurika katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane 2026 yanayoendelea Nzuguni, Dodoma, ambapo wanapata fursa ya kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayotekelezwa na Wakala nchini.

Mbali na kupata elimu kuhusu teknolojia za nishati safi ya kupikia, wageni wanaotembelea banda la REA wanaelezwa kuhusu mchango wa miradi hiyo katika kulinda mazingira, kuboresha afya za wananchi, kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, pamoja na kuongeza ustawi wa jamii.
REA inaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake ili kujionea huduma na fursa mbalimbali zinazotolewa na Wakala katika kuendeleza upatikanaji wa nishati endelevu nchini.

