MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Habari

Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu, Dodoma

Programu ya Mama Samia ya Utambuzi na Urasimishaji Ujuzi imezinduliwa rasmi ikiwa na lengo la kuwawezesha vijana wenye ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi kutambuliwa na kurasimishwa, ili kuongeza fursa za ajira ndani na nje ya nchi.

Tayari vijana 14400 wamenufaika na program hiyo, huku lengo likiwa ni kuwafikia vijana 30,000 kwa mwaka huu wa 2026/27.

Akizindua program hiyo inayoratibiwa na Mamlaka Ya Ufundi Stad Tanzania (VETA), Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema ujuzi ni mali, mtaji na nguvu ya taifa, na hivyo ni muhimu kwa vijana kujitokeza ili kutathminiwa na kurasimishwa.

Habari Picha 11900

Amesema kupitia programu hiyo ya Mama Samia, serikali inatambua kwamba kumpa kijana cheti cha ufundi stadi siyo tu kumpa karatasi, bali ni kumpa hadhi, sauti na nafasi ya kushindana katika soko la ajira

Ameongeza kuwa programu hiyo inatekelezwa kimkakati ili kuhakikisha mafundi hawalazimiki kusafiri umbali mrefu, kwani huduma zitawafikia walipo, na kwamba anachotakiwa fundi ni kuwasilisha maombi kupitia ofisi za Halmashauri au v

yuo vya VETA vilivyo karibu na hakuna gharama yoyote atakayotakiwa kulipa wakati wa urasimishaji.

Ameongeza kuwa waajiri wanapaswa kuwa tayari kushirikiana na vijana watakaopata vyeti kupitia mpango huo, ambao unalenga kukuza ajira na ujuzi rasmi nchini.

Habari Picha 11901

Aidha, amebainisha kuwa vyeti vinavyotolewa kwa kundi hilo la vijana vinatokana na umahiri wao na vigezo vilivyowekwa na VETA, kupitia miongozo ya kitaaluma.

“Si kila mwenye ujuzi anarasimishwa moja kwa moja, bali hufanyiwa tathmini, na endapo kuna mapungufu husaidiwa kwa mafunzo ya ziada ili kukidhi viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Ameongeza kuwa cheti cha VETA kinatambulika rasmi na kinampa mhitimu nafasi ya kuaminika katika soko la ajira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), CPA Anthony Kasore, amebainisha kuwa lengo la programu hiyo ni kuwafikia wananchi 80,000 kufikia mwaka 2027.

Habari Picha 11904

 

 

Amesema kwa mwaka huu pekee, serikali imelenga kuwafikia wananchi 30,000, ambapo tayari imepatiwa fedha kwa ajili ya kuwafikia wananchi 14,400 bila malipo yoyote kwa wanufaika.

Amesema kuwa serikali imetoa takriban sh milioni 600 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli hiyo, na kwamba baada ya kukamilisha awamu ya kwanza, wataendelea na waliobaki ili kufikia lengo lililowekwa.

Ameongeza kuwa programu hiyo itaongeza ajira na fursa mbalimbali kwa wananchi baada ya kupata vyeti vinavyotambulika rasmi.

You Might Also Like

Tanzania Na Africa50 Wazidi Kuimarisha Ushirikiano

Balozi Seokolo Atoa Wito Kuimarisha Biashara na Viwanda Kanda ya SADC

Kilimo Shadidi Kinapunguza Uzalishaji Wa Gesi

Jeshi la polisi kumhoji anayesambaza taarifa za uongo

TAWIA na MAIPAC washirikiana kuadhimisha Siku ya Wajane, wapanga kupanda Mlima Kilimanjaro

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TEA, Wizara ya Elimu Zanzibar Kushirikiana Kuimarisha Miradi ya Elimu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TEA, Wizara ya Elimu Zanzibar Kushirikiana Kuimarisha Miradi ya Elimu
Habari April 23, 2026
Bajeti Yadhihirisha Uhakika Wa Nishati Nchini
Habari April 23, 2026
Ushirikiano wa TEA, Halmashauri wapewa msukumo kuimarisha mifuko ya elimu
Habari April 22, 2026
Kisima Kimoja Cha Gesi Chaonesha Mshangao Kwa Uzalishaji Wa Gesi-PURA
Habari April 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?