MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yaweka Mkazo Kufufua Viwanda Musoma Ili Kuongeza Ajira
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yaweka Mkazo Kufufua Viwanda Musoma Ili Kuongeza Ajira
Habari

Serikali Yaweka Mkazo Kufufua Viwanda Musoma Ili Kuongeza Ajira

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imeeleza kuimarisha jitihada za kufufua viwanda vilivyokwama uzalishaji ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi, hususan katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema hatua hiyo inakuja kutokana na tathmini pamoja na mazungumzo yaliyofanyika kati ya Serikali na wawekezaji kuhusu hatima ya viwanda vilivyokuwa vimesimama kwa muda mrefu.
Amebainisha kuwa makubaliano yamefikiwa kurejesha Kiwanda cha MUTEX kwa mwekezaji wa awali kwa masharti mapya, huku mkataba ukiwa tayari umefanyiwa uhakiki na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuwasilishwa kwa Msajili wa Hazina kwa hatua zaidi.
Kwa mujibu wa Londo, maboresho ya mwisho ya mkataba huo yanaendelea kukamilishwa kabla ya kukabidhiwa rasmi kwa mwekezaji ili aanze uzalishaji bila kuchelewa.
Kuhusu Kiwanda cha Musoma Dairy, amesema mwekezaji wa awali ameonyesha nia ya kurejea kuendesha shughuli za uzalishaji, na kwamba Serikali inaendelea kupitia ombi hilo kabla ya kufikia uamuzi.
Amekiri kuwa kwa sasa viwanda vya MUTEX na Musoma Dairy havifanyi kazi, jambo linalopunguza fursa za ajira kwa wakazi wa eneo hilo, lakini akasisitiza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha vinafufuliwa haraka kwa manufaa ya wananchi.
Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Musoma Mjini, Mgore Kigera, Londo ameuliza kama mchakato wa mkataba mpya unaweka masharti yatakayomhakikishia mwekezaji kuanza uzalishaji kwa wakati.
Pia ameeleza kuwa Serikali haina taarifa zozote kuhusu vitendo vya wizi katika Kiwanda cha Musoma Dairy.

You Might Also Like

Mfumo wa Usalama Majumbani, Umewakumbuka Wenye Ulemavu

Tido Mhando: Marufuku Kuwasilisha Vyeti, Nyaraka Za Kughushi Maombi ya Ithibati, Press Card

Mongella Atoa Maagizo Maalum Kwa Viongozi CCM

Matumizi Ya Baiteknolojia Nchini ni Madogo – Profesa Yanda

‘Upungufu wa Wakunga Afrika Watishia Maisha ya Mama na Mtoto ‘TAMA

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Habari April 23, 2026
TEA, Wizara ya Elimu Zanzibar Kushirikiana Kuimarisha Miradi ya Elimu
Habari April 23, 2026
Bajeti Yadhihirisha Uhakika Wa Nishati Nchini
Habari April 23, 2026
Ushirikiano wa TEA, Halmashauri wapewa msukumo kuimarisha mifuko ya elimu
Habari April 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?