MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Miaka 40 ya Costech: Ruzuku ya Ubunifu Imegeuza Wazo Kuwa Kiwanda Cha Kimataifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Miaka 40 ya Costech: Ruzuku ya Ubunifu Imegeuza Wazo Kuwa Kiwanda Cha Kimataifa
Makala

Miaka 40 ya Costech: Ruzuku ya Ubunifu Imegeuza Wazo Kuwa Kiwanda Cha Kimataifa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
7 Min Read
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu wakiwa kwenye uzinduzi wa ‘Premier Products’ uliofanyika Arusha mwaka juzi 2024
Na Lucy Ngowi
MWAKA 2015, vijana watatu wenye ndoto ya kutatua changamoto za wakulima walikuwa na wazo tu.
Hawakuwa na kiwanda, hawakuwa na mashine za kisasa wala mtaji mkubwa. Walichokuwa nacho ni ubunifu na imani kwamba teknolojia inaweza kubadilisha kilimo cha Tanzania.
Leo, miaka 11 baadaye, kampuni yao ya Imara Technology Ltd imeajiri zaidi ya watu 50, imesambaza mashine zaidi ya 2,500 ndani na nje ya Tanzania, imefikia zaidi ya wakulima 100,000 na kuuza bidhaa zake katika nchi nane za Afrika.
Nyuma ya mafanikio hayo kuna uwekezaji wa Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), taasisi inayoadhimisha miaka 40 tangu kuanzishwa kwake.
Habari Picha 13137

Mkurugenzi mtendaji wa Imara Tech Alfred Chengula

Mkurugenzi Mtendaji wa Imara Technology Ltd, Alfred Chengula, anasema safari yao ilianza kwa kupata ruzuku ya kwanza ya COSTECH iliyowawezesha kutengeneza mfano (prototype) wa mashine yao ya kwanza.

“Tulikuwa na wazo pekee. COSTECH ilitupa ruzuku ya kwanza iliyotuwezesha kutengeneza mashine yetu ya kwanza na kuijaribu. Baadaye tukapata ruzuku nyingine kwa ajili ya kufanya utafiti wa soko kabla ya kuingia rasmi sokoni,” anasema Chengula.
Fedha hizo hazikusaidia tu kutengeneza mashine, bali pia zilitoa ujasiri wa kuanzisha kampuni rasmi mwaka 2019.
Kutoka kwa wabunifu watatu, leo Imara Technology imekua kampuni inayotengeneza teknolojia za kilimo zinazotambulika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Chengula anasema mashine yao maarufu ina uwezo wa kukoboa na kupura mazao tisa tofauti, yakiwemo mahindi, maharage, mtama, mbaazi, alizeti, choroko na uwele. Ubunifu huo umeondoa ulazima wa kuwa na mashine tofauti kwa kila zao, hivyo kupunguza gharama kwa  na wajasiriamali.
Kampuni hiyo pia hutengeneza mashine za kutengeneza chakula cha mifugo zinazokatakata mabua, kusaga magunzi na kuandaa malighafi mbalimbali kwa ajili ya lishe ya mifugo.
Kwa mujibu wa Chengula, mafanikio hayo yasingefikiwa bila mazingira yaliyowekwa na COSTECH ya kuwalea wabunifu kutoka hatua ya wazo hadi biashara.
“Tulianza kwa ruzuku ya Sh. Milioni 20, baadaye tukapata Sh. Milioni 40 kwa ajili ya kuendeleza teknolojia yetu. Zaidi ya fedha, COSTECH ilinipa fursa ya kwenda Finland kukutana na wawekezaji. Safari hiyo ilizaa uwekezaji wa zaidi ya Sh. milioni 500 kwenye kampuni yetu,” anasema.
Kwa miaka 40, COSTECH imekuwa kiungo kati ya utafiti, ubunifu, mtaji na masoko, ikiwezesha mawazo ya Watanzania kukua na kuwa biashara zinazochangia uchumi wa taifa.
Leo, mashine za Imara Technology zimeuzwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rwanda, Uganda, Burundi, Kenya, Malawi na Zimbabwe. Zaidi ya mashine 300 zimeuzwa nje ya Tanzania, jambo linaloonyesha kuwa teknolojia ya Kitanzania inaweza kushindana katika soko la kikanda.
Chengula anasema siri ya mafanikio yao ni kubuni teknolojia zinazojibu mahitaji halisi ya wakulima. Mashine hizo ni rahisi kubebwa hata kwa pikipiki, hutumia mafuta kidogo na zina uwezo wa kukoboa gunia 25 za mahindi kwa saa kwa kutumia lita moja tu ya mafuta, huku zikimwezesha mjasiriamali kupata hadi Sh. 25,000 kwa saa.
Hata hivyo, anasema sekta ya ubunifu bado inakabiliwa na changamoto za gharama kubwa za malighafi kutokana na kodi za pembejeo na uhaba wa wataalamu wa kuendesha mashine za kisasa.
Licha ya hayo, kampuni ina mpango wa kujenga kiwanda kikubwa Dodoma kitakachoongeza uzalishaji, ajira na ushindani wa teknolojia za kilimo za Tanzania.
Lakini mafanikio ya Imara Technology hayaishii kiwandani. Yanaonekana pia mashambani, ambako teknolojia hiyo imebadili maisha ya wakulima.
Mkurugenxi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu aliwahi kunukuliwa akisema, “Teknolojia hii inawasaidia wakulima wadogo kufanya kazi kwa haraka na kuongeza kipato,”.
Pia alisifu ubunifu wa kampuni hiyo
 kwa kutengeneza mashine ya kisasa ya kupuria mazao mbalimbali.
Habari Picha 13135
Timu ya Imara Tech ikiwa Ruvuma
Ikitoa elimu ya mashine kwa wakulima
Miongoni mwa wanufaika ni mkulima Raphael Mwazembe wa Wilaya ya Mbozi.
Anasema alianza kutumia mashine za Imara Technology mwaka 2018, wakati kampuni hiyo ikiwa ndiyo inaanza kujijengea jina sokoni. Tangu wakati huo, uzalishaji wake umeongezeka na biashara yake imepanuka.
“Nilipoona uwezo wake wa kufanya kazi nilikamilisha malipo na kuanza kuitumia. Baada ya muda wakulima wengine walivutiwa nayo kwa sababu wakati huo hakukuwa na mashine nyingine yenye uwezo kama huo,” anasema.
Mkulima huyo anasema, kutokana na mafanikio aliyoyapata, baadaye alinunua mashine kubwa zaidi na kuanza kutoa huduma kwa wakulima, ikiwemo nchini Kenya. Pia aliongeza mashine ya kubangua na kusaga nafaka kwa ajili ya kutengeneza chakula cha kuku na mifugo mingine.
Mwazembe, ambaye pia ni mtengenezaji wa mashine anasema mashine hizo zimemwezesha kuzalisha malisho bora na kuwavutia wakulima wengi kufuata huduma zake.
Anaongeza kuwa matoleo mapya ya mashine hizo yameboreshwa zaidi na yana uwezo mkubwa wa kuongeza uzalishaji.
Anawahimiza wakulima kutumia mashine zenye ubora uliothibitishwa, akieleza kuwa alizonunua zimeendelea kufanya kazi kwa ufanisi kwa miaka mingi.
Kwa mujibu wake, mashine hiyo ina uwezo wa kuchakata gunia moja la mahindi ndani ya takribani dakika moja, kutegemeana na kasi ya upakiaji.
Maelezo ya Mwazembe yanaonyesha kwa vitendo jinsi uwekezaji wa COSTECH ulivyosaidia kubadili wazo la wabunifu wa Kitanzania na kuwa teknolojia, inayoboresha maisha ya maelfu ya wakulima.
Kutoka kwenye ruzuku ya kutengeneza mfano wa kwanza wa mashine hadi kufikia mauzo katika nchi mbalimbali za Afrika, Imara Technology ni ushahidi kwamba uwekezaji katika sayansi, teknolojia na ubunifu unaweza kuzalisha ajira, kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi wa taifa.
Huo ndio urithi wa miaka 40 ya COSTECH kuibua vipaji, kukuza ubunifu na kugeuza mawazo ya Watanzania kuwa suluhisho zinazogusa maisha ya wananchi na kuipa Tanzania nafasi ya ushindani katika uchumi wa maarifa.
  • Habari Picha 13139

Timu ya Mafundi ya Imara Tech wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukamilisha toleo jipya la mashine kubwa ya kuchakata chakula cha mifugo

 

You Might Also Like

Teknolojia ya Kuvuna Sumu ya Nyuki Yafungua Fursa Mpya Tanzania

Shen Zhiying: Mkongwe Aliyeanzisha Kozi Ya Kiswahili Nchini China

Ushirikiano Wa Afrika, China Kuonyesha Mwelekeo Maendeleo Ya Dunia

Kutoka Wazo Rahisi Hadi Mapinduzi ya Kilimo: Safari ya Rafiki Planter Inayosimulia Miaka 40 ya COSTECH

Kila Parachichi, Ndizi au Chungwa Ninalouza ni Tiketi Ya Matumaini Ya Watoto Wangu – Beatrice

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mfumo Wa Kidijitali Wa PSSSF Wamvutia Mkurugenzi Wa BOT
Next Article COSTECH Yapambania Haki Za Wabunifu, Yalenga Kupeleka Bunifu Sokoni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

DC Kondoa  Aipongeza TFS Kwa Teknolojia Ya Uhifadhi Wa Misitu Na Utali
Habari August 8, 2026
Waziri Nanauka Aipongeza   TARURA Kwa Mpango Wa  CBRM ‎
Habari August 8, 2026
PURA Yawataka Watanzania Kujenga Uwezo Kunufaika Na Sekta Ya Mafuta Na Gesi
Habari August 8, 2026
COSTECH Yapambania Haki Za Wabunifu, Yalenga Kupeleka Bunifu Sokoni
Habari August 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?