MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: COSTECH Yapambania Haki Za Wabunifu, Yalenga Kupeleka Bunifu Sokoni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > COSTECH Yapambania Haki Za Wabunifu, Yalenga Kupeleka Bunifu Sokoni
Habari

COSTECH Yapambania Haki Za Wabunifu, Yalenga Kupeleka Bunifu Sokoni

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: SERIKALI imeongeza nguvu katika kulinda haki za wabunifu nchini kwa kuweka mifumo itakayowawezesha vijana kusajili, kulinda na kufanya bunifu zao kuwa bidhaa za kibiashara, huku ikisisitiza kuwa ubunifu ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi wa taifa.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wabunifu hawapotezi fursa kutokana na ukosefu wa ulinzi wa haki miliki na changamoto za kufikisha teknolojia zao sokoni.
Dkt. Nungu ameyasema hayo baada ya kutembelea Banda la Vijana linaloshiriki Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (BBT) katika Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa ya Kilimo (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samweli Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.
Amesema COSTECH imekuwa ikijenga mazingira wezeshi kwa wabunifu kupitia utoaji wa fedha za kuanzia, dhamana za mikopo pamoja na kuwaunganisha na taasisi mbalimbali ili kupata mitaji na fursa za kibiashara.
“Serikali haitoi fedha pekee kwa wabunifu, bali inajenga mfumo unaowasaidia kulinda kazi zao, kuziboresha na kuzifikisha sokoni,” amesema.
Amesema katika mazungumzo na wabunifu vijana, wamebaini changamoto mbalimbali ikiwemo usajili wa kampuni, utambulisho wa bidhaa na upatikanaji wa vibali, ambazo zinahitaji kushughulikiwa kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali.
Dkt. Nungu amesema moja ya maeneo yanayopewa kipaumbele ni ulinzi wa haki miliki za wabunifu, akieleza kuwa bunifu isiyolindwa inaweza kupoteza thamani yake na kuwanyima wabunifu manufaa yanayotokana na kazi zao.
Ametolea mfano kijana aliyebuni teknolojia ya kutengeneza mbolea kwa kutumia nywele, ambaye baada ya kupata msaada wa COSTECH katika usajili na ulinzi wa haki zake za ubunifu, aliweza kupata uwekezaji na fedha kutoka nje ya nchi.
“Hii inaonyesha umuhimu wa kuwa na mifumo ya kuwawezesha wabunifu kuanzia hatua ya wazo hadi kufikia soko,” amesema.
Aidha, amesema COSTECH imepokea maombi ya vijana kuhusu changamoto za marejesho ya mikopo inayotolewa na halmashauri, ambapo wameomba muda wa kuanza kulipa uongezwe ili kuwapa nafasi ya kuendeleza miradi yao.
Amesema suala hilo litajadiliwa na mamlaka husika ili kuboresha mazingira ya mikopo kwa vijana wabunifu na wajasiriamali.

You Might Also Like

Timu Ya Watanzania Ikiongozwa Na Profesa Ndunguru, Yakutana Na Balozi Zambia

Walimu Ni Nguzo ya Maadili na Uzalendo kwa Taifa – Rais CWT

Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti

VETA Yajipanga Kutoa Mafunzo Yanayoendana na Teknolojia ya Kisasa

Trilioni 11.5 Zimetumika Miradi Ya Maendeleo Kigoma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Miaka 40 ya Costech: Ruzuku ya Ubunifu Imegeuza Wazo Kuwa Kiwanda Cha Kimataifa
Next Article PURA Yawataka Watanzania Kujenga Uwezo Kunufaika Na Sekta Ya Mafuta Na Gesi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

DC Kondoa  Aipongeza TFS Kwa Teknolojia Ya Uhifadhi Wa Misitu Na Utali
Habari August 8, 2026
Waziri Nanauka Aipongeza   TARURA Kwa Mpango Wa  CBRM ‎
Habari August 8, 2026
PURA Yawataka Watanzania Kujenga Uwezo Kunufaika Na Sekta Ya Mafuta Na Gesi
Habari August 8, 2026
Miaka 40 ya Costech: Ruzuku ya Ubunifu Imegeuza Wazo Kuwa Kiwanda Cha Kimataifa
Makala August 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?