Na Lucy Lyatuu,Dodoma
MAMLAKA Ya Udhibiti Mkondo Wa Juu Wa Petroli (PURA) imesema imekamilisha uchimbaji wa kisima kimoja cha uchimbaji gesi cha Mnazi Bay Mtwara ambacho kimeonesha maajabu kwa kuwa na uwezo wa kuzalisha gesi futi za ujazo milioni 45 Kwa siku.

Mkuu wa Kitengo Cha Uhusishwaji Wa wazawa na wadau kutoka PURA,Charles Nyangi amesema hayo wakati akitoa taarifa Kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, anayeshughulikia mafuta na gesi asilia,Dkt James Mataragio alipotembelea Banda la Mamlaka hiyo katika wiki ya Nishati inayoendelea katika viwanja vya Bunge.
Amesema uchimbaji wa visima ni hatua iliyokuwa ikitekelezwa na Mamlaka hiyo na kwamba kisima hicho kilichokamilika awali kilitarajiwa kuzalisha futi za ujazo milioni 20 Kwa siku jambo ambalo limekuwa ni tofauti na matarajio.
“Imekuwa ni mshangazo mkubwa kwetu, na hii ndio inaonyesha kuwa ipo akiba kubwa ya gesi nchini,” amesema Nyangi na kuongeza kuwa kisima lingine linaendelea na hatua za uchimbaji.

Amesema kisima hicho kimebakia mita 1500 kukamilika na kwamba hatuabalimbali za utafiti wa gesi zinaendelea katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
ipo akiba kubwa ya gesi,ikiwa ni baada ya kukamilika

