MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kamati Ya Bunge Yatoa Maelekezo Ya Usimamizi Wa Kodi Kwa  Kwa TRA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kamati Ya Bunge Yatoa Maelekezo Ya Usimamizi Wa Kodi Kwa  Kwa TRA
Habari

Kamati Ya Bunge Yatoa Maelekezo Ya Usimamizi Wa Kodi Kwa  Kwa TRA

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Lyatuu,Dodoma
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imeelekeza Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kuchukua hatua za haraka kurekebisha mapungufu yote yaliyoibuliwa na Mdhibiti Na Mkaguzi Mkuu Wa Hesabu Za Serikali CAG, hususan katika maeneo ya ukusanyaji wa kodi na usimamizi wa mapato ya serikali.

Mwenyekiti wa PAC, Devotha Minja, amesema hayo baada ya Kamati kukutana na Menejimenti ya TRA kwa ajili ya kupokea, kupitia na kuchambua taarifa ya hesabu za taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2025, zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Habari Picha 12356

Katika kikao hicho, PAC imeielekeza TRA kuchukua hatua za haraka kurekebisha mapungufu yote yaliyoibuliwa na CAG, hususan katika maeneo ya ukusanyaji wa kodi na usimamizi wa mapato ya serikali.

Akizungumza, Minja ameeleza kuwa Kamati imeitaka TRA kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa kodi kwa kuongeza ufanisi katika ukaguzi, uhakiki wa taarifa za walipakodi, pamoja na kuboresha mifumo ya ufuatiliaji wa mapato ili kuhakikisha hakuna upotevu wa fedha za umma.

Amesema Kamati inamtaka Ofisa Maduhuri kuwasilisha taarifa ya kiasi cha kodi kilichokusanywa kufikia June 30,2024 na June 30,2025 na taarifa hiyo ifanyiwe usahihi na CAG na kuwasilishwa Kwa Kamati ifikapo Agosti 30,2026.

Habari Picha 12357

Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, amesema taasisi hiyo imepokea maelekezo yote ya PAC na kuyapa kipaumbele, na akiahidi kuwa mapungufu yaliyobainishwa yatashughulikiwa ndani ya muda uliopangwa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TRA, Uledi Mussa, amesema kikao hicho kimekuwa fursa muhimu ya kujifunza na kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa zaidi ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi na walipakodi.

Ameongeza kuwa lengo la TRA ni kuwa taasisi inayoaminika na wananchi, huku ikiendelea kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari kama njia ya kuongeza mapato ya ndani na kuchochea maendeleo ya taifa.

Kadhalika ameiomba PAC kuendelea kuwa mabalozi wa kuelimisha na kuhamasisha wananchi kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari .

Habari Picha 12358

You Might Also Like

Mpango wa Shule Salama Unaongeza ulinzi Kwa Watoto

TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge

TUGHE: Wafanyakazi wapewe haki ya kujiunga vyama vya wafanyakazi

Msigwa Awataka Wakuu Wa Mikoa Kuandaa Maeneo Ya Upandaji Miti

Wachimbaji Wadogo Wafikiwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tume Ya Ulinzi Wa Taarifa Binafsi Yatoa Siku Saba Kwa Taasisi Kujisajili
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume Ya Ulinzi Wa Taarifa Binafsi Yatoa Siku Saba Kwa Taasisi Kujisajili
Habari June 12, 2026
Teknolojia Ya Juisi YA Ndizi Kali Yafungua Fursa Mpya Za Viwanda, Ajira
Makala Uncategorized June 12, 2026
Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?