MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TADB Yapongezwa Kwa Kuuongeza Uzalishaji Wa Mazao Nchini,Kuinua Kipato
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TADB Yapongezwa Kwa Kuuongeza Uzalishaji Wa Mazao Nchini,Kuinua Kipato
Habari

TADB Yapongezwa Kwa Kuuongeza Uzalishaji Wa Mazao Nchini,Kuinua Kipato

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu, Dodoma
WAZIRI Mkuu ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Kwamba uwekezaji wake umeendelea kuongeza uzalishaji wa mazao,kuimarisha usalama wa chakula na kuinua kipato cha wananchi.
Ameipongeza benki hiyo kwa mchango wake katika kuimarisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini, huku akiitaka kuongeza uwezo wa kifedha ili kuwafikia wakulima wengi zaidi na kuharakisha mageuzi ya uzalishaji wa chakula na mazao ya biashara.
Mwigulu amesema hayo baada  ya kutembelea banda la TADB katika Maonesho ya Nanenane  jijini Dodoma.
Habari Picha 12997
 Amesema Serikali inahitaji kuona TADB ikijengewa uwezo mkubwa zaidi wa kifedha ili iwe chanzo cha uhakika cha mitaji kwa sekta ya kilimo, akibainisha kuwa utegemezi wa ruzuku pekee hauwezi kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya wakulima nchini.
Ameitaka TADB kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na TAMISEMI kuwekeza katika ujenzi wa maghala ya kuhifadhi mazao ili kuboresha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, hatua itakayowawezesha wakulima kuhifadhi mazao yao, kuyatumia kama dhamana ya mikopo na kuuza wakati bei zinapokuwa nzuri.
“Maboresho hayo yataongeza tija katika biashara ya mazao, kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuongeza thamani ya uzalishaji wa wakulima,” amesema.
Akizungumza, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Frank Nyabundege, amesema benki hiyo imeendelea kufadhili miradi ya kimkakati inayobadilisha sekta ya kilimo nchini, ikiwemo umwagiliaji, mazao ya biashara na miradi ya kuongeza thamani ya mazao.
Habari Picha 13010
Amesema zaidi ya sh bilioni 700 zimetolewa kufadhili miradi ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali nchini, huku vyama vya ushirika vinavyozalisha kahawa, hususan katika mikoa ya Kagera na Kigoma, vikiwa miongoni mwa wanufaika wakubwa wa huduma za kifedha zinazotolewa na benki hiyo.
Nyabundege amesema TADB pia imewezesha mradi wa kisasa wa uzalishaji na uchakataji wa samaki uliopo Bagamoyo, unaotumia teknolojia ya kisasa iliyopatikana kutoka Misri, ambayo kwa sasa ina uwezo wa kuhifadhi hadi tani 90 za samaki kwa mwezi kwa kuzingatia viwango vya utunzaji wa mazingira.
Amesema mradi huo umefungua soko kubwa la samaki, umeongeza thamani ya mazao ya uvuvi na umeifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi za kwanza katika ukanda kutumia teknolojia hiyo ya kisasa katika sekta ya uvuvi.
“Tunaendelea kufanya vizuri katika kufadhili miradi yenye tija kwa uchumi wa nchi. Lengo letu ni kuhakikisha sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi zinakuwa nguzo kuu za maendeleo ya uchumi,” amesema Nyabundege.

You Might Also Like

Waziri Mkuu Aagiza Kuimarisha Ufuatiliaji Na Tathmini Kuleta Maendeleo

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni

Ridhiwani Kikwete Atembelea Banda la REA, Aipongeza Kasi ya Usambazaji Umeme Vijijini

FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara

Rais Samia ashuhudia JOWUTA Ikiwa mwanachama wa  TUCTA 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article SmartDarasa: Tunda la Miaka 40 ya COSTECH Linalobadili Elimu ya Sayansi Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

SmartDarasa: Tunda la Miaka 40 ya COSTECH Linalobadili Elimu ya Sayansi Tanzania
Makala August 1, 2026
TVLA Yazalisha Chanjo ya Kudhibiti Homa ya Kutupa Mimba kwa Mifugo
Habari August 1, 2026
Halmashauri Ya Jiji La Dodoma Lawataka Wakulima Kutumia Nanenane Kujifunza Kilimo Cha Kisasa
Habari August 1, 2026
Dkt. Nchemba: TPHPA Yazidi Kuwafikia Wakulima
Habari August 1, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?