MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TSB yaanzisha ‘special’ Mkonge BBT
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TSB yaanzisha ‘special’ Mkonge BBT
Habari

TSB yaanzisha ‘special’ Mkonge BBT

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DODOMA: BODI ya Mkonge Tanzania (TSB) imeanzisha mradi maalumu wa Jenga Kesho iliyo Bora kupitia Zao la Mkonge (Special Mkonge BBT) ambayo inahusisha makundi ya wanawake, vijana na wenye ulemavu.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge, Saddy Kambona amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la TSB kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nanenane kwenye Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Amesema mradi huo unahusisha uongezaji thamani wa zao la mkonge ambapo makundi hayo hupewa mafunzo ya kuzalisha bidhaa za mkono kupitia zao la mkonge.
Amesema mkonge una manufaa mengi lakini kwa uchache unao mnyororo wake wa thamani ambapo katika program hiyo maalumu ya BBT wanawaweka pamoja makundi maalumu yakiwamo ya wanawake na vijana na kuwapa mafunzo ya jinsi ya kuzalisha bidhaa za mikono kupitia zao la mkonge.
“Lakini kwa vijana tunajua kwenye eneo la ujenzi bidhaa nyingi za ujenzi zinaweza kuzalishwa na vijana kama kuzalisha ‘gypsum board’ kwa kutumia nyuzi za mkonge.
“Kwa hiyo vijana hii ni fursa nzuri ya kujitengenezea ajira kupitia zao la mkonge kwa sababu tutakuwa na vituo atamizi maalumu kwenye mikoa ya Tanga, Morogoro na Dodoma kwa Tanzania Bara.
“Upande wa Zanzibar kwenye Chuo cha Mafunzo Zanzibar ambapo tutakuwa tunawapelekea nyuzi za mkonge na kuendesha mafunzo kujifunza njia mbalimbali za kuzalisha bidhaa zenye ubora tupate manufaa ya kujipatia ajira, kipato na kubadilisha hali za maisha yetu,” amesema Kambona.
Mradi huo ambao umezinduliwa rasmi Julai 27, mwaka huu Visiwani Zanzibar unasimamiwa na TSB kwa kuashirikiana na Wizara ya Viwanda na Uchumi wa Buluu, Wizara ya Maliasili na Mali Kale na Chuo cha Mafunzo Zanzibar.
Mradi huo tayari umeanza kufanya kazi kwa kutoa mafunzo na kugawa mkonge tani 9.6 zenye thamani ya Sh milioni 40 kwa vikundi 20 vya wanawake, vijana na wenye ulemavu visiwani humo.

You Might Also Like

TARI Yakutanisha Wadau Afya Ya Udongo

Hakuna Mabadiliko Ya Vituo Vya Kazi Kwa Watumishi Wapya Wa Umma Kwa Sasa -Kikwete

Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima

TEA Yakabidhi Miradi Iliyokamilika Wilayani Mtama, Masasi

UDSM Yashirikiana na China Kukuza Maarifa na Urafiki Kupitia Vitabu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article SIDO jengeni viwanda 20 Kila mkoa-Jafo
Next Article Homa ya nyani mjadala wa dharura kwa mawaziri wa afya Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mkutano wa Mawaziri wa SADC Wahitimishwa Pretoria
Habari March 13, 2026
Tanzania, Afrika Kusini Zakubaliana Kuharakisha Makubaliano ya Ushirikiano
Habari March 13, 2026
Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Habari March 12, 2026
Mamlaka Za Mitaa Ondoeni Urasimu Katika Kuanzisha Biashara Mpya-Waziri Mkuu
Habari March 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?