MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rita Kabati Aahidi Kuimarisha Miundombinu, Kuwatumikia Wananchi Wa Kilolo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rita Kabati Aahidi Kuimarisha Miundombinu, Kuwatumikia Wananchi Wa Kilolo
Habari

Rita Kabati Aahidi Kuimarisha Miundombinu, Kuwatumikia Wananchi Wa Kilolo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Jimbo la Kilolo, Rita Kabati (CCM), amesema katika Bunge la 13 anatarajia kufanyika kwa mabadiliko makubwa yatakayowaletea wananchi maendeleo ya kweli.
Amesema hayo nje ya viwanja vya Bunge alipozungumza na Waandishi wa Habari katika Mkutano wa Kwanza  wa Bunge la 13, Dodoma.
Amesema tayari amefanya tathmini ya changamoto zilizopo katika vijiji vyote vya jimbo hilo na amejiandaa kuzitafutia ufumbuzi kupitia vikao vya Bunge na ushirikiano na serikali.
“Nimekuwa mbunge ninayeuliza maswali mengi yenye maslahi kwa wananchi, jambo lililowajengea imani kwamba ninawapigania kwa dhati. Sasa naenda kutekeleza yale yote niliyokuwa nikiyasema bungeni,” meisema Kabati.
Mbunge huyo amebainisha kuwa changamoto kubwa katika jimbo la Kilolo ni barabara zisizopitika wakati wa mvua, hali inayokwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii.
“Niliahidi kwa wananchi wangu kuwa nitahakikisha maeneo korofi yanatengenezwa ili barabara ziweze kupitika muda wote. Tayari upembuzi yakinifu umefanyika, hivyo kazi inaanza mara moja,” amesisitiza.
Kabati amesema hatakwenda bungeni kwa maneno matupu bali kwa vitendo, akisisitiza kuwa dhamira yake ni kutumikia wananchi kwa uaminifu na uadilifu.
“Siji kuremba, nakuja kazini. Wananchi wameniamini, nami nitahakikisha sitawaangusha. Tunataka kuwaonyesha Watanzania kuwa wanawake wanaweza, na tunataka idadi ya wabunge wanawake wa majimbo iongezeke kwa sababu tunafanya kazi,” amesema.

You Might Also Like

TARI: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Yamepunguza Ufanisi Wa Mbegu

Ofisi Zote Dodoma Kutoa Ushirikiano Kwa Watangazaji-RC

SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele

MAIPAC Yagawa Makoti Ya Usalama Kwa Wanahabari Kuelekea Uchaguzi Mkuu.

TARI Kihinga Yainua Kilimo Cha Michikichi Kigoma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Chatanda Ampongeza Samia, Aahidi Kuinua Wanawake Kiuchumi
Next Article Chiku Athumani Aahidi Kusimamia Afya na Elimu kwa Umakini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
Ufaulu  Wa   Somo La Hisabati  Shida Ya Taifa- Wanu
Habari April 16, 2026
Ofisi ya Rais Mipango Yaomba Bilioni 144.85 kwa Bajeti 2026/27
Habari April 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?