Na Lucy Lyatuu, Dodoma
MFUKO wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umesema unaratibu mradi wa awamu ya 10 ambao utawezesha ujenzi wa minara 287 ambao utaongezq huduma za mawasiliano nchi nzima.
Meneja Mradi wa UCSAF, Mhandisi Wilfred Charles amesema hayo wakati akizungumza na vyombo vya habari katika maonesho ya Utumishi wa Umma mkoani Dodoma.
Mhandisi Charles amesema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo umechangia zaidi asilimia 50 ya huduma za mawasiliano na intanet vijijini.

Aidha amefafanua wanatoa mafunzo kwa tehema kwa walimu ili kuweza kuwasaidia kutekeleza majukumu yao katika masomo ya Tehama ambayo mpango huo unaendana pamoja na dira ya 2050.
Kuhusu hali ya mawasilino kwa sasa nchini amesema wameshatoa huduma ya mawasiliano vijijini wakijenga minara 2000 vijijini na mradi wa minara 758 nchini kote mijini na vijijini tayari umekamilika.
‘ Tumefikia shule zaidi ya 1000tukipeleka kompyuta ili waweze kupata huduma ikiwa ni za sekondari, msingi hata vyuo,” amesema Charles na kuongezw kuwa wanatumia wiki ya utumishi wa umma kutoa elimu kuhusu ,ajukumu yao.

