MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wiki ya Huduma za Fedha: SELF Yafungua Fursa za Kiuchumi kwa Wananchi Tanga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wiki ya Huduma za Fedha: SELF Yafungua Fursa za Kiuchumi kwa Wananchi Tanga
Habari

Wiki ya Huduma za Fedha: SELF Yafungua Fursa za Kiuchumi kwa Wananchi Tanga

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
TANGA: WANANCHI wametakiwa kuwa waangalifu na wenye uelewa wa kutosha wanapochukua mikopo ili kuepuka kuingia kwenye mzigo wa madeni usio na tija, hususan mikopo yenye riba kubwa inayodaiwa kuwanyonya wananchi.
Wito huo umetolewa na Meneja Masoko na Uhamasishaji wa Mfuko wa SELF, Linda Mshana, leo Januari 20, 2026, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha yanayoendelea katika viwanja vya Usagara, jijini Tanga.
Maadhimisho hayo yalianza Januari 19 na yanatarajiwa kumalizika Januari 26, 2026.
Mshana amesema mfuko wa SELF unaendelea kutoa elimu sahihi ya fedha kwa wananchi, ikiwemo matumizi bora ya mikopo, mambo ya kuzingatia kabla ya kuchukua mkopo pamoja na maswali muhimu ya kuuliza wanapohusiana na taasisi za kifedha,
Hatua itakayowasaidia kuepuka changamoto za mikopo isiyo rafiki.
Ameongeza kuwa wananchi wa mkoa wa Tanga wanakaribishwa kufika katika maadhimisho hayo ili kupata elimu ya fedha, kufahamu fursa zilizopo pamoja na kujifunza njia mbalimbali za kujiendeleza kiuchumi.
Kwa mujibu wa Mshana, SELF ina mikopo ya aina mbalimbali inayolenga makundi tofauti yakiwemo wafanyabiashara wa nafaka, wafugaji, wavuvi na wakulima.
Aidha, mfuko huo pia hutoa mikopo ya kuboresha makazi kwa wananchi wanaotaka kuboresha nyumba zao ili zipate muonekano bora zaidi.
“Kwa wale wanaotaka kuanzisha au ambao tayari wanaendesha taasisi za kifedha zinazotoa mikopo na wamepata kibali cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT), SELF inatoa fursa ya kuongeza mtaji kupitia mikopo,” amesema.
Amebainisha kuwa suala la riba limekuwa likiulizwa mara kwa mara, hali inayoonesha kuwa bado kuna uhitaji mkubwa wa elimu kuhusu namna sahihi ya kukokotoa riba na kuelewa gharama halisi za mikopo.
Mshana ameongeza kuwa mafunzo hayo yanatolewa kupitia mfuko wa SELF kwa lengo la kuwajengea wananchi uelewa mpana wa masuala ya kifedha.
Amesema mfuko wa SELF ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Fedha, inayojikita katika kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo yenye masharti nafuu, sambamba na kutoa elimu ya fedha na bima.

You Might Also Like

Benjamin Mkapa Yaanzisha Mfuko Kuchangia Wagonjwa Wa Upandikizaji Figo,Uloto Wasiokuwa Na Uwezo

Majaliwa awasili Kilimanjaro kufungua semina Mambo ya Ndani

Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030

MOI Kuendesha Kambi Maalum Ya Uchunguzi,  Ushauri Wa Kitabibu Kwa Wazee

Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mwenyekiti Wa Kijiji Aahidi Kufuatilia Mgogoro wa Shamba Bahi
Next Article TIRA Yasisitiza Umuhimu wa Bima katika Kulinda Uchumi wa Taifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TTCL  Yatumia Tamasha La Kizimkazi Kueleza  Wananchi Fursa Wanazotoa
Makala August 15, 2026
Rais Samia Afurahishwa Na Huduma za NSSF
Habari August 13, 2026
  VETA Yashiriki Tamasha La Kizimkazi
Habari August 13, 2026
Vijana Watakiwa Kuanza Utekelezaji Wa Mipango Waliyonayo
Habari August 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?