MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanataaluma Wahimizwa Kutumia Tafiti Kama Chachu ya Mabadiliko ya Jamii
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanataaluma Wahimizwa Kutumia Tafiti Kama Chachu ya Mabadiliko ya Jamii
Habari

Wanataaluma Wahimizwa Kutumia Tafiti Kama Chachu ya Mabadiliko ya Jamii

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Vincent Mpepo (OUT)
WANATAALUMA katika taasisi za elimu ya juu nchini wamehimizwa kubadili mtazamo wao kuhusu tafiti kwa kuzitumia kama nyenzo ya kuleta mabadiliko chanya ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni, badala ya kuziona kama hitaji la kitaaluma pekee la kukamilisha masomo.
Wito huo umetolewa lna washiriki wa mafunzo ya siku mbili ya ushauri wa kitaalamu yanayoendelea katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), jijini Dar es Salaam, yakihusisha wanataaluma kutoka Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii pamoja na vitivo vingine.
Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mtiva wa Kitivo, Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Ustawi wa Jamii, Dkt. Mariana Makuu, amesema kuwa ni wakati wa wanataaluma kubadili mwelekeo kutoka tafiti za kinadharia kwenda kwenye tafiti zenye matokeo halisi kwa jamii.
Amebainisha kuwa mafunzo hayo yanalenga kuongeza umahiri wa ushauri wa kitaalamu, hatua itakayosaidia kutatua changamoto za jamii, kuongeza mapato na kuimarisha taswira ya taasisi.
Habari Picha 10703
Kwa upande wake, mwezeshaji wa mafunzo, Innocent Deus, amesema kuwa tafiti zinapaswa kuelekezwa katika kutatua changamoto halisi za jamii ili kuongeza thamani ya taaluma na kuhalalisha mchango wa wanataaluma mbele ya wadau wa maendeleo.
Amesisitiza pia umuhimu wa ushirikiano kati ya wanataaluma na taasisi zenye uzoefu ili kuimarisha ubunifu na fursa za miradi.
Akichangia mjadala, Dkt. Janeth Laurean amependekeza kuwepo kwa utaratibu wa kuwatambua wanataaluma wabunifu watakaobuni tafiti zitakazoingizia chuo mapato.
Aidha, imebainika kuwa bado kuna mtazamo kwa baadhi ya wasomi wa kuiona elimu kama njia ya kuhitimu tu, badala ya chombo cha kuleta mabadiliko ya kweli katika jamii.
Habari Picha 10704
Habari Picha 10705

You Might Also Like

Tulia Atoa Taarifa Kifo Cha Ndugai

CHAUMMA: Tupo Tayari Kupunguza Gharama za Maisha – Salum Mwalim

Pato la Mwananchi Lapanda Tabora

TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar

UDOM yashauri matumizi ya green house kupata tija

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Yasema Migogoro Ya Ndoa lliyotatuliwa Imeongezeka
Next Article Serikali Yatumia Teknolojia Kuwaunganisha Vijana Na Fursa Za Kiuchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
Ufaulu  Wa   Somo La Hisabati  Shida Ya Taifa- Wanu
Habari April 16, 2026
Ofisi ya Rais Mipango Yaomba Bilioni 144.85 kwa Bajeti 2026/27
Habari April 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?