MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Bunge Bonanza 2026 Kuikutanisha Simba Na Yanga Dodoma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Bunge Bonanza 2026 Kuikutanisha Simba Na Yanga Dodoma
Habari

Bunge Bonanza 2026 Kuikutanisha Simba Na Yanga Dodoma

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MWENYEKITI wa Bunge Sports Club, Festo Sanga, ametangaza kufanyika kwa Bunge Bonanza 2026 kubwa litakalowakutanisha mashabiki wa timu kongwe za Simba na Yanga, lililoandaliwa na Benki ya Azania.
Bonanza hilo linatarajiwa kufanyika Januari 31, 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin, jijini Dodoma.
Akizungumza  na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Bunge Msekwa, Sanga alisema bonanza hilo linalenga kuhamasisha michezo, afya na mshikamano, huku mashabiki wa Simba na Yanga wakikutana kwa amani, furaha na burudani.
Habari Picha 10970
Alisema mashabiki wa michezo wanakaribishwa kushiriki na kushuhudia jumla ya michezo 21 itakayochezwa siku hiyo, ikiwemo mchezo wa mpira wa miguu kati ya Simba na Yanga pamoja na michezo mingine ya burudani na afya.
Sanga aliongeza kuwa mgeni rasmi katika Bunge Bonanza 2026 atakuwa Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba.
Alisema kutakuwa na maandamano ya amani yatakayoanza saa 12 asubuhi, yakielekea katika viwanja vya John Merlin ambako bonanza hilo litafanyika.
Aidha, Benki ya Azania imethibitishwa kuwa mdhamini mkuu wa bonanza hilo kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.
Akizungumza kuhusu ushiriki wa benki hiyo, Meneja Mahusiano wa Benki ya Azania, Elizabeth Nyatega, alisema michezo ina mchango mkubwa katika kukuza afya ya jamii.
Habari Picha 10972
“Benki ya Azania itaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge na wadau wa michezo katika kukuza sekta ya michezo, vipaji na afya za Watanzania,” alisema Nyatega.
Aliongeza kuwa siku ya bonanza, benki hiyo itatoa huduma zote za kibenki kwa ajili ya kuwahudumia washiriki na wageni watakaohudhuria.
Katika hatua nyingine, Nyatega alikabidhi vifaa mbalimbali vya michezo kama sehemu ya maandalizi ya kuelekea Bunge Bonanza 2026.

You Might Also Like

Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu

Serikali Kuimarisha Uvuvi Bahari Kuu Kupitia TAFICO

Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa

Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM

Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waziri Mkuu Asisitiza Elimu ya Bima ya Afya kwa Wote Vijijini
Next Article Hakuna Mabadiliko Ya Vituo Vya Kazi Kwa Watumishi Wapya Wa Umma Kwa Sasa -Kikwete
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mabilika Kutoka Ubunifu Hadi Soko La Afrika
Makala August 9, 2026
TARURA Yafungua Njia Mpya Kukwepa Msongamano Dodoma
Habari August 9, 2026
TPHPA Kuja Na Ramani Ya Visumbufu Nchi Nzima
Habari August 9, 2026
Dkt. Samia: Ushirika Simamieni Matrekta Kwa Manufaa Ya Wakulima
Habari August 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?