MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yatumia Teknolojia Kuwaunganisha Vijana Na Fursa Za Kiuchumi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yatumia Teknolojia Kuwaunganisha Vijana Na Fursa Za Kiuchumi
Habari

Serikali Yatumia Teknolojia Kuwaunganisha Vijana Na Fursa Za Kiuchumi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: SERIKALI imesema inaendelea kutumia teknolojia kama nyenzo muhimu ya kuharakisha utoaji wa huduma, kupokea maoni na kuwaunganisha vijana na fursa za kiuchumi, kijamii kwa urahisi na kwa wakati.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka amesema serikali imeanza maandalizi ya kuanzisha jukwaa la kidijitali la huduma jumuishi litakalowezesha vijana kupata taarifa za ajira, mafunzo, mikopo, masoko na huduma nyingine kwa mfumo rahisi.
Amesema pia serikali inaendelea kuimarisha majukwaa ya ushiriki wa vijana ikiwemo VIJANA Platform, linalolenga kusikiliza sauti za vijana, kujadili changamoto zao na kuwaunganisha na wadau, sambamba na kukamilisha mifumo ya kisheria ya ushiriki wa vijana ikiwemo Baraza la Vijana.
Nanauka amesema serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya ubunifu kwa vijana kupitia vituo atamizi na kulea wabunifu pamoja na kuimarisha ulinzi wa kazi za ubunifu katika sanaa, michezo, filamu na muziki ili vijana wanufaike kiuchumi.
Aidha, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana ina vituo vitatu vya maendeleo ya vijana vya Sasanda (Songwe), Ilonga (Morogoro) na Marangu (Kilimanjaro), ambavyo vimepangwa kufufuliwa na kuboreshwa ili kutoa ujuzi wa vitendo, ujasiriamali na ajira, ikiwemo kuanzisha programu ya Open Coding School kwa ujuzi wa TEHAMA.
Amesisitiza kuwa utekelezaji wa ajenda ya vijana unahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo sekta binafsi, taasisi za fedha, mashirika ya kiraia na wadau wa maendeleo.
Amewahimiza vijana kuwa wazalendo, wachapakazi na walinzi wa amani, akisisitiza kauli mbiu ya “Vijana Tuyajenge, Tanzania ni Yetu” kama wito wa vitendo katika kujenga Taifa.

You Might Also Like

Kanisa lakabidhi jengo la watoto la milioni 595 kwa serikali

Serikali Yachukua Hatua Madhubuti Kukuza Ajira kwa Wahitimu wa Vyuo

Makala: Hakuna Kupita Bila Kupingwa

Manara: Sitapambana na Wafanyabiashara, Nitawatetea

WMA Yajivunia Kuongezeka Kwa Wafanyakzai

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanataaluma Wahimizwa Kutumia Tafiti Kama Chachu ya Mabadiliko ya Jamii
Next Article Lugha ya Kichina Ni Ufunguo wa Fursa za Kimataifa – Profesa Maisel
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
Ufaulu  Wa   Somo La Hisabati  Shida Ya Taifa- Wanu
Habari April 16, 2026
Ofisi ya Rais Mipango Yaomba Bilioni 144.85 kwa Bajeti 2026/27
Habari April 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?