Na Lucy Lyatuu,Morogoro
MAMLAKA Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi Stad (VETA) Dakawa Morogoro imeandaa mpango maalum wa kufundisha wafugaji ili kutunza vizuri mifugo jambo litakalosaidia kipandisha thamani ya ngozi.
Mwalimu Wa Bidhaa Za Ngozi kutoka VETA Dakawa Morogoro,Hamidu Nahembe amesema hayo wakati akizungumza katika banda la Mamlaka hiyo lililoko kwenye tamasha la nne la kitaifa la utamaduni linalofanyika mkoani Morogoro.
Amesema kupitia tamasha hilo wanaelimisha wananchi kuhusiana na utamaduni kupitia fani ya ngozi,ambapo VETA inafundisha vijana kuhusu maadili yanahoihusu ngozi katika kukuza utamaduni.



” Tumekuja pia kueleza wafugaji kuhusu umuhimu wa utamaduni kuhusu namna ya kutunza ngozi jambo litakalopandisha hadhi na thamaninya ngozi hata katika bidhaa zitokanazo na ngozi”, amesema na kuongeza kuwa thamani ya ngozi hupanda pale mifugo inapotunzwa vizuri.
Amesema wafugaji hawatakiwi kuweka alama kwa mfugo katika sehemu zisizofaa akitolea mfano kutowekwa kwa vifaa ambavyo vinaweza kukwaruza mifugo ovyo badala yake wawatumie watalaam kupata elimu ya.msingi na maelekezo ya maeneo yanayostahili kuweka alama
Nahembe amesema alama zinawekwa sehemu zisizoleta madhara ambazo ni pamoja na mwisho wa mguu ama kwenye sikio, hivyo wanakumbusha wafugaji kujenga mabanda ambayo ni bora yanayotunza vizuri ngozi za wanyama wao.
Kadhalika amewataka kutojenga mabanda yenye seng’enge kwa kuwa yanaweza kukwarua ng’ombe kwenye miili yao na kufifisha ubora wa ngozi au kujenga mabanda yenye miiba ambayo sio salama kwenye ubora wa ngozi wajenge ya mabanzi.
Amesema ni muhimu mfugaji kutambua kuwa ngozi moja inaweza kutoa viatu pea 15 hadi 20 hivyo inaweza kusababisha kupafa faida hadi sh 600,000,jambo ambalo wafugaji hawalijui.
Kuhusu tamasha hilo amesema wana bidhaa zilizoboreshwa na kwamba vyema kupata watalam huo na kupata ngozi yenye thamani na ubora.


