Na Lucy Lyatuu,Dodoma
WAKALA wa Barabara Mijini Na Vijijini (TARURA) imesema imeanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilomita 1.6 unaoanzia eneo la TRA kuelekea King’ong’o eneo la Kimara Mwisho jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano Na Mawasiliano Kwa Umma wa TARURA, Catherine Sungura amebainisha hayo katika wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma.
Amesema mpaka sasa imebakia kilomita 1.6 ya ujenzi wa Barabara hiyo na kwamba katika mwaka wa fedha 2026/2027 kipande Cha mita 800 kitakuwa kimefikiwa.
“Meneja wa wilaya ya Ubungo amethibitisha kuwa kilomita 1.6 za Barabara ndizi zimebakia na mwaka ujao wa fedha atajenga mita 800 ambazo zitaweza kuunganisha na maeneo mengine,” amesema Sungura na kuongeza kuwa majivu hayo yametokana na mwananchi alifika katika Banda hilo na kuuliza kuhusu ujenzi wa Barabara hiyo.

Amesema wamekuwa waliotumia wiki hiyo kutoa elimu Kwa wananchi kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Barabara katika maeneo hayo na kuwaunganisha Kwa simu na mameneja wa sehemu husika Ili kupata majibu.
Amesema wananchi wengi wanafika katika Banda hilo wakitaka kujua ukamilishwaji wa Barabara na kwamba watafikiwa lini na hata kuhusu ujenzi wa Barabara mpya zitakazofunguliwa.
” Tume kuwa tukiwaelimisha kuhusu Barabara mpya kwenye maeneo yao na kwamba wasijenge kwenye eneo la Barabara,” amesema na kuongeza kuwa ni vyema wafahamu kuwa TARURA inajenga Barabara za lami,vumbi,changarawe na zege.
Amesisitiza kuwa TARURA itaendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara inaboreshwa ili kurahisisha mawasiliano na usafiri kwa wananchi, huku akieleza kuwa barabara bora zinachochea upatikanaji wa huduma za kijamii, biashara na shughuli nyingine za maendeleo.
Kuhusu wiki hiyo amesema zaidi ya wananchi 300 wametembelea banda la TARURA tangu kuanza kwa Wiki ya Utumishi wa Umma, wakipata elimu na ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara katika maeneo yao, hatua hiyo imeendelea kuimarisha uhusiano kati ya wananchi na taasisi hiyo huku ikitoa fursa ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi moja kwa moja.


