MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TUCTA Yawataka Wanahabari Kueneza Elimu ya Fidia kwa Wafanyakazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TUCTA Yawataka Wanahabari Kueneza Elimu ya Fidia kwa Wafanyakazi
Habari

TUCTA Yawataka Wanahabari Kueneza Elimu ya Fidia kwa Wafanyakazi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
RAIS wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya amesema waandishi wa habari wana nafasi kubwa ya kuelimisha jamii kuhusu huduma zinazotolewa na taasisi mbalimbali za umma na binafsi, ikiwemo Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Nyamhokya ameitoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo kuhusu fidia kwa wafanyakazi kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanaofanya Kazi katika Vyombo vya Habari (JOWUTA), yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Mei 25, 2026.
Amesema mafunzo hayo yameandaliwa kwa ushirikiano na WCF kwa lengo la kuongeza uelewa kwa wanahabari kuhusu haki, mafao na taratibu za fidia kwa wafanyakazi ili waweze kuripoti masuala hayo kwa usahihi kwa umma.
Habari Picha 12230
Kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WCF, John Mduma, Nyamhokya ameishukuru JOWUTA kwa juhudi zake za kuwaunganisha wanachama na kuwajengea uwezo kupitia mafunzo hayo muhimu.
Ameeleza kuwa WCF ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria kwa ajili ya kuwahudumia wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi wanaopata ajali, kuugua au kufariki kutokana na kazi zao.
Habari Picha 12231
Aidha, amesema mfuko huo unatoa mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, fidia ya ulemavu wa muda na kudumu, msaada kwa wategemezi wa marehemu pamoja na huduma za utengemao.
Nyamhokya amewataka wanahabari kutumia taaluma yao kuwahamasisha waajiri kujisajili WCF na kuwasilisha michango kwa wakati, huku pia wakielimisha wafanyakazi umuhimu wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi ili kuimarisha mshikamano katika kutetea haki na maslahi yao.
Habari Picha 12232

You Might Also Like

Simbachawene: Nitaheshimu Mfumo Wa Uongozi Na Kushirikiana

Kamati Ya Bunge Yapongeza Usimikaji Mfumo Wa Kidijitali CMA

Mpango Wa Taifa Wa Teknolojia Uko Mbioni Kuja-Serikali

Serikali Kuwasilisha Bungeni Nyenzo Kuu Tatu Zitakazowezesha Utekelezaji Dira 2050

BRELA Yatwaa Tuzo Sabasaba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article JOWUTA Yataka Wanahabari Wasajiliwe WCF
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

JOWUTA Yataka Wanahabari Wasajiliwe WCF
Habari May 26, 2026
Teknolojia ya Kuvuna Sumu ya Nyuki Yafungua Fursa Mpya Tanzania
Makala May 25, 2026
NIDA Kufanya Usajili Wa Watoto  Kuanzia Umri Wa Kuzaliwa,Kutoa Namba Maalum
Habari May 25, 2026
TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari May 24, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?