MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TUCASA Yatoa Mapendekezo ya Sheria, Sera Kwa Serikali Kutatua Ucheleweshaji Wa Malipo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TUCASA Yatoa Mapendekezo ya Sheria, Sera Kwa Serikali Kutatua Ucheleweshaji Wa Malipo
Habari

TUCASA Yatoa Mapendekezo ya Sheria, Sera Kwa Serikali Kutatua Ucheleweshaji Wa Malipo

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHAMA cha Makandarasi na Watoa Huduma za Kikandarasi (TUCASA), kimeiomba serikali kuchukua hatua madhubuti kuzuia ucheleweshaji wa malipo kwa makandarasi wanaotekeleza miradi ya maendeleo nchini.

Msemaji wa TUCASA Harris Kapiga, amesema hayo alipozungumza na Waandishi wa Habari alipokuwa akielezea kuhusu kufanyika kwa kongamano lijulikanalo kama TUCASA Day 2025 litakalofanyika kuanzia Septemba mbili hadi tatu, mwaka huu, 2025 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Kapiga ametaja mapendekezo mengine ya chama hicho ni pamoja na kutungwa kwa Sheria ya Malipo itakayolazimisha malipo kufanyika ndani ya muda maalum wa kisheria kwa miradi ya ujenzi.

Pia chama hicho kimetaka kuanzishwa kwa Dhamana ya Malipo, ambapo taasisi zote za serikali zinazotoa mikataba ya ujenzi zitoe dhamana kwa makandarasi ili kuondoa mashaka ya kucheleweshwa kwa fedha.

“TUCASA pia imeitaka serikali kuanzisha sera maalum za kuongeza ushiriki wa wakandarasi wa ndani katika miradi mikubwa ya kitaifa ili kupunguza utegemezi kwa wakandarasi wa nje,” amesema.

Msemaji wa huyo wa TUCASA,  Kapiga amesema hadi sasa deni kwa makandarasi limefikia Sh. Trilioni 1.20, ambapo makandarasi wa ndani wanadai Bilioni 190, kati ya hizo Bilioni 115 ni kwa miradi iliyokamilika, na Bilioni 75 kwa miradi inayoendelea.

Akinukuu Kamati ya Bunge ya Miundombinu, amesema kufikia Februari 2025, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ulikuwa na deni la Sh. Trilioni 1.20, linalojumuisha malipo kwa wakandarasi wa ndani, wa nje, na riba ya ucheleweshaji wa malipo.

Kapiga amesema, “Makandarasi ndio msingi wa maendeleo ya miundombinu. Nyumba unayoishi, daraja unalopita, umeme unaotumia kuchaji simu, yote yana mkono wa mkandarasi. Ucheleweshaji wa malipo kwa makandarasi ni sawa na kusimamisha ujenzi wa taifa. Tunahitaji suluhisho la kitaasisi na kisheria,”.

Amesema kwa kipindi cha miaka minne, deni kwa makandarasi limekuwa likiongezeka sambamba na bajeti ya Wizara ya Ujenzi. Katika bajeti ya mwaka 2025/2026, Serikali imeidhinisha Sh. Trilioni 2.28 kwa Wizara ya Ujenzi ongezeko la asilimia 28 kutoka bajeti ya mwaka uliopita.

Kwa mwaka 2024 pekee, Sh. Bilioni 507.759 zilihusiana na miradi inayoendelea, huku Bilioni 652.213 zikiwa ni madeni ya miradi iliyokamilika lakini haijalipwa.

Kuhusu kongamano hilo ametaja kauli mbiu yake inayosema, ‘Makandarasi na Watoa Huduma Wazawa ni Nguzo ya Uchumi wa Taifa’.

Mkutano huo utawakutanisha makandarasi na watoa huduma kutoka maeneo mbalimbali nchini kujadili changamoto zinazowakabili, ikiwa ni pamoja na ucheleweshwaji wa malipo, mikataba yenye masharti magumu, na utegemezi wa makandarasi wa nje.

 

 

 

 

You Might Also Like

China Yaendelea Kunufaisha Afrika, Wakati Marekani Ikikatiza Uwekezaji Katika Bara Hilo

Aprili 2025 Matokeo Awamu Ya Kwanza, Maoni Dira Ya Taifa Na Maendeleo 2050 Kutolewa

TEN/MET, LHRC Zataka Iwekwe Marufuku Matumizi Ya Viboko

Hazina yaanza kuwalipa wanachama 465 wa TALGWU

Walimu Kupatiwa Mafunzo ya Tehama

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Aweka Jiwe La Msingi Kongani Ya Kwala
Next Article Asha Moto Aibuka Kidedea Ubunge wa Viti Maalum Mtwara Kupitia CCM
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Habari August 1, 2025
Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Habari August 1, 2025
Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Habari August 1, 2025
Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini
Habari July 31, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?