MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TBA Yaongeza Elimu kwa Wananchi Kuhusu Huduma na Miradi ya Uwekezaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TBA Yaongeza Elimu kwa Wananchi Kuhusu Huduma na Miradi ya Uwekezaji
Habari

TBA Yaongeza Elimu kwa Wananchi Kuhusu Huduma na Miradi ya Uwekezaji

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zake mbalimbali na miradi ya uwekezaji inayotekelezwa nchini kupitia ushiriki wake katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma.
Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa TBA, Lumuli Mwangosi, amesema taasisi hiyo inatumia fursa hiyo kuwafahamisha wananchi kuhusu majukumu yake pamoja na huduma zinazotolewa kwa lengo la kuboresha ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa.
Amesema TBA hutoa huduma za ushauri wa ujenzi wa majengo ya serikali, upangishaji wa nyumba za watumishi wa umma na ofisi, pamoja na kushiriki katika utekelezaji wa miradi ya uwekezaji kwa kushirikiana na sekta binafsi.
Kwa mujibu wa Mwangosi, wakala huo unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali katika mikoa tofauti ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, huku ukitumia maonesho hayo kuwaelimisha wananchi kuhusu fursa zinazopatikana kupitia miradi hiyo.
“Wananchi wanaotembelea banda letu wanapata nafasi ya kufahamu huduma tunazotoa, kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali na kujionea hatua za miradi inayotekelezwa na TBA,” amesema.
Ameeleza kuwa kaulimbiu ya mwaka huu ya ‘Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu’ inaakisi dhamira ya taasisi hiyo ya kuhakikisha watumishi wake wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi, uwazi na uwajibikaji ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Aidha, amesema TBA imeendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali katika shughuli zake za kila siku ili kuongeza ufanisi na kurahisisha utendaji kazi.
Baadhi ya mifumo inayotumika ni pamoja na Watumishi Portal, Mrejesho, Msawazo, mifumo ya mikopo pamoja na mfumo wa usimamizi wa utendaji kazi wa PePMIS.
Mwangosi ameongeza kuwa taasisi hiyo inaendelea kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kupitia mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu yanayolenga kuongeza ujuzi wa watumishi na kuwawezesha kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia pamoja na mahitaji ya kisasa ya utoaji huduma.
Amesema mafunzo hayo yanawahusisha watumishi wa kada mbalimbali, wakiwemo wahandisi na watumishi wa utawala, kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi na kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi.

You Might Also Like

Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu

Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88

Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’

Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia

Wafanyakazi wa Majumbani Wajengewa Uwezo 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article WRRB YATOA FURSA MPYA KWA WAFUGAJI NCHINI
Next Article Serikali Yaitaka TBS Kuongeza Ubunifu, Usasa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mfumo Wa Kidijitali Wa PSSSF Wamvutia Mkurugenzi Wa BOT
Habari August 5, 2026
FAO Yasisitiza Kutowapa Mifugo Dawa Bila Maelekezo Ya Watalaam
Habari August 5, 2026
Balozi Wa Kudumu Wa Mashirika Ya UN Atembelea FAO Nanenane
Habari August 5, 2026
Wadau Wamiminika Banda La REA Katika Maonesho Ya Nanenane  2026
Habari August 5, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?