MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi
Habari

TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read

Yazalisha Miche Bora na Kufundisha Wakulima

Na Lucy Ngowi

MOROGORO: Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) imesema licha ya kuwepo kwa teknolojia mbalimbali za kuboresha kilimo cha minazi, bado wadau wengi hawajaweza kuzijua wala kuzifikia.

Akizungumza katika Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki, Mratibu wa Uhaulishaji wa Teknolojia na Mahusiano kutoka Kituo cha TARI Mikocheni, Vidah Mahava, amesema wameanzisha mkakati maalum wa kufufua na kuendeleza kilimo cha minazi nchini kwa kutumia mbinu mbalimbali.

Hatua kubwa zilizochukuliwa na kituo hicho ni kuzalisha mbegu bora, kutoa mafunzo kwa wakulima, na kuanzisha vitalu vya miche katika maeneo mbalimbali nchini.

Hata hivyo, changamoto kubwa ni ukosefu wa taarifa na elimu sahihi kwa wakulima kuhusu teknolojia za kisasa za minazi, zikiwemo mbegu bora, kanuni za upandaji, na udhibiti wa magonjwa na wadudu waharibifu kama vile mbu wa minazi na chonga.

Baadhi ya wakulima hulima minazi bila kufuata kanuni, huku wengine wakishindwa kutambua tofauti kati ya kole lenye ugonjwa na lenye afya.

Ugonjwa wa kunyong’onyea umetajwa kuwa tishio kubwa kwa minazi, lakini wengi hawana elimu ya kuutambua na kuukabili. Ili kuhakikisha teknolojia hizi zinawafikia wananchi,

TARI kupitia Kituo cha Mikocheni kinaendelea kuzalisha miche bora ya minazi kwenye vitalu. Tayari miche imepelekwa kwa awamu mbili katika mikoa ya Lindi na Mtwara, kutokana na ombi la wananchi kwa Rais Samia Suluhu Hassan alipowatembelea.

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na 2024/2025, miche yote iliyozalishwa kwenye vitalu vya vituo vidogo vya TARI Mikocheni iligawiwa kwa wananchi.

Pamoja na kuzalisha miche katika vituo hivyo, juhudi zimefanyika kuanzisha vitalu vya pamoja kati ya TARI na halmashauri za mikoa inayolima minazi nchini. Vitalu hivyo vimeanzishwa katika Halmashauri za Ruangwa (Lindi), Muheza (Tanga), na Mtwara Vijijini (Mtwara).

Halmashauri hizi tatu zilipokea mbegu 6,000 kila moja, ambazo tayari ziliota na kugawiwa kwa wakulima ndani ya halmashauri zao. Aidha, TARI Mikocheni kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mkinga (Tanga) wameanzisha kitalu cha pamoja chenye mbegu 6,000 ambazo bado ziko ardhini mpaka zitakapokuwa tayari kugawiwa.

Mazungumzo yanaendelea baina ya TARI na Halmashauri ya Same (Kilimanjaro) kwa ajili ya kupeleka mbegu zaidi. Mpango wa upandaji wa minazi unafanyika kwa uwiano wa mita 10 kwa 10, ambapo ekari moja hupandwa miti 40, na kila mti una uwezo wa kutoa nazi 35 hadi 40 kwa mwaka.

Mbali na minazi, kituo hicho kinaendelea na utafiti wa maabara kwa ajili ya utambuzi wa magonjwa ya minazi na mazao mengine, pamoja na kuzalisha miche kwa kutumia teknolojia za kisasa (kwa njia ya chupa) kwa mazao kama mananasi, mihogo, viazi vitamu, na mkonge.

Mojawapo ya mafanikio mapya ni teknolojia ya uzalishaji wa mananasi aina ya MD2 kwa njia ya chupa. Mananasi haya ni bora kwa Biashara, yanafaa kwa juisi, yana ladha tamu, hayaozi haraka, na yana soko kubwa ndani na nje ya nchi iwapo uzalishaji utakuwa wa kutosha.

7Mashamba darasa ya mananasi haya yalifanyika Bagamoyo (Pwani), Kinole (Morogoro), na Madeke (Njombe).

Kupitia mafunzo kwa wakulima, vijana, wanawake, na wazee, TARI Mikocheni inalenga kuhakikisha teknolojia hizi haziishii kwenye maonesho ya kilimo, bali zinamfikia mkulima wa kawaida vijijini.

You Might Also Like

Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025

Hakuna Mabadiliko Ya Vituo Vya Kazi Kwa Watumishi Wapya Wa Umma Kwa Sasa -Kikwete

RC Chalamila, Wasaidizi Wake Kukutana na Kadogosa Kuzungumzia Ujenzi Wa Reli Dar

Mbunge Msita Ataka Ukarabati Wa Haraka Barabara Zilizoharibiwa Na Mvua

Wanafunzi Kutoka Veta Kushiriki Mafunzo Japan

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tari Ilonga yaboresha mbegu, mavuno yapanda hadi tani 3.8 kwa hekta
Next Article Serikali Yawekeza Katika Utafiti wa Alizeti, Wakulima Wapate Mbegu Bora
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari May 24, 2026
Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Habari May 22, 2026
Biashara 15 Hazitakiwi Kufanywa Na Wageni Ndani Ya Nchi
Habari May 22, 2026
Wadau wataka mifumo jumuishi kupunguza mzigo wa malezi kwa wenye ulemavu
Habari May 21, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?