Na Lucy Lyatuu,Dodoma
SERIKALI imesema iko tayari kushughulikia utitiri wa vyama vingi vya sekta binafsi Ili kuwa na mwavuli mmoja ulio imara na makini na Wenye kufanya vizuri.
Waziri wa Nchi Ofisi Ya Rais Mipango Na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema hayo wakati akizungumza na viongozi wa sekta binafsi jijini hapa.
Amesema kumekuwepo na changamoto ya mkanganyiko wa sekta binafsi na kwamba lazima Serikali ishuhulikie suala hilo Ili kwamba Kila mmoja ajiunge na Taasisi ya sekta binafsi Iliyo imara.

Amesema lengo la kufanya hivyo ni Ili kufanya vizuri ambapo katika mkutano huo wadau hao wametakiwa kuendeleza muundo ambao utawezesha kuwa na ushirikiano na sekta binafsi na kuwa na miongozo itakayofuatwa na Wenye kutoa matokeo.
” Katika muundo huo tuwe na namna ya kutatua changamoto ambazo tunakutana nazo ziweze kutatuliwa ikiwemo za kiutawala au kiutendani,” amesema Profesa Mkumbo na kuongeza kuwa hio ni namna ya kusimamia mipango ya nchi na nna ya kuongeza uwekezaji.
Amesema lengo la kukutana na viongozi wa sekta hizo ni katika kufahamiana na kuyajua majukumu ya Wizara hio ikiwa ni pamoja na kuratibu programu za kuondoka umaskini,kuhamasisha uwekezaji,kusimamia na kuratibu maendeleo ya sekta binafsi lakini pia kuhakikisha mazingira ya biashara yanaimarishwa.

Amesema katika malengo ya Wizara hiyo inahitajika kuwa na sekta binafsi Iliyo imara na kwamba serikali inaendelea kushughulikia vikwazo vyote vinavyokwaza sekta hiyo pamoja na mazingira yake.
Akizungumza NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya Ya Wafanyabiashara Tanzania (JWTZ), Ismail Masoud amesema IPO haja Kwa Wizara hiyo kuweka mipango itakayowezesha Uchumi wa Nchi kukua Kwa Kasi na kuepuka kufanya kazi kwa mazoea.
Amesema sekta binafsi unaweza kukuza Uchumi na kufikia asilimia 15 lakini ni muhimu kufanya kazi kwa pamoja na ukiritimba kuondolewa Kwa baadhi ya watawala.

