MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: OUT: Elimu Sasa Kiganjani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > OUT: Elimu Sasa Kiganjani
HabariUncategorized

OUT: Elimu Sasa Kiganjani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
CHUO Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kimeendelea kutumia teknolojia za kisasa kubadili mfumo wa utoaji wa elimu, kuwawezesha wanafunzi kusoma wakiwa katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi bila kulazimika kufika chuoni.
Hatua hiyo imeifanya elimu ya masafa kuwa sehemu muhimu ya utoaji wa elimu katika chuo hicho, huku wanafunzi wakitumia majukwaa ya kidijitali kujifunza, kuwasiliana na walimu na kufanya mitihani kulingana na mifumo inayotumiwa na chuo.
Habari Picha 13421
Akizungumza katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, Mkurugenzi wa Huduma za Wanafunzi wa OUT, Dkt. Zacharia Rwejuna, amesema chuo hicho kimeendelea kuboresha mifumo ya utoaji wa elimu kwa kutumia teknolojia za mtandao.
Amesema OUT inatoa programu kuanzia ngazi ya cheti hadi shahada ya uzamivu (PhD), zinazofundishwa kwa njia ya masafa na mtandao, hivyo kuwawezesha wanafunzi kuendelea na majukumu yao huku wakisoma.
“Katika maonyesho haya tumeleta programu zetu zinazotolewa kuanzia ngazi ya cheti hadi shahada ya uzamivu (PhD). Programu hizi zinafundishwa kwa njia ya masafa na mtandao, hivyo aina hii ya usomaji inaleta chachu ya ubunifu katika elimu,” amesema.
Dkt. Rwejuna amesema hapo awali wanafunzi walitegemea zaidi matini za kujisomea kabla ya kufika katika vituo vya mikoa kufanya mitihani, lakini mfumo huo umeendelea kuboreshwa kupitia matumizi ya majukwaa ya kidijitali, yakiwemo Moodle na Zoom.
Habari Picha 13422
Amesema majukwaa hayo yanawawezesha wanafunzi kuwasiliana na walimu na kushiriki vipindi vya masomo kwa njia ya mtandao, hatua inayopanua fursa za elimu kwa Watanzania na wadau waliopo nje ya nchi.
“Ubunifu tulio nao unalenga kuongeza ujuzi na tija katika ufundishaji, pamoja na kuwafikia wananchi wengi katika maeneo mbalimbali. Ubunifu huo unaonekana katika namna tunavyofundisha, tunavyofanya mitihani na hata katika mchakato wa usahihishaji,” amesema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ubunifu wa OUT, Dkt. Straton Ruhinda, amesema chuo hicho kinaendelea kuboresha mitaala yake ili kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaozingatia vitendo na mahitaji ya soko la ajira.
Habari Picha 13423
Amesema mfumo huo unawafaa watu wenye majukumu mbalimbali, kwa kuwa mwanafunzi anaweza kusoma akiwa mahali popote kwa kutumia kompyuta au simu janja, mradi awe na huduma ya mtandao.
Dkt. Ruhinda amesema kupitia mfumo wa ODEX, wanafunzi wanapata fursa ya kufanya mitihani kwa wakati unaowafaa kulingana na majukumu yao.
Amewahimiza wananchi kutumia fursa zinazotolewa na OUT kupata elimu, akisema matumizi ya teknolojia za kisasa yanaendelea kurahisisha upatikanaji wa elimu na kuwawezesha wanafunzi kufikia malengo yao.

You Might Also Like

SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.

Mpanduji Wa COTWU – T Aelezea Changamoto Zinazowakabili Waendesha Bodaboda, Bajaji

WRRB Kuanza Kuingiza Sekta Ya Mifugo Kwenye Mfumo Wa Stakabadhi Za Ghala

Serikali Yaahidi Kupatia Dawa Kilio Cha Ushuru Kwa Malori

Wizara Ya  Ujenzi Kutekeleza Vipaumbele Sita,Ujenzi Wa Miundombinu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article NGARUMA VTC  Kutoa Mafunzo Katika Fani Mbalimbali Za Ufundi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NGARUMA VTC  Kutoa Mafunzo Katika Fani Mbalimbali Za Ufundi
Habari August 24, 2026
VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine
Habari August 23, 2026
Airtel Yajenga Darasa La Fursa Katika Shule Ya Sekondari Magaoni,Tanga
Habari August 23, 2026
Bunifu ya dawa ya mayai yapunguza hasara kwa wafugaji wa kuku
Makala August 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?