MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine
Habari

VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
SERIKALI kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema itaendelea kutoa fursa za mafunzo ya ufundi kwa watu wenye mahitaji maalum na kugharamia ada zao, ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha kupata ujuzi wa kujitegemea.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Anthony Kasore, amemtaka mhitimu wa kozi fupi ya useremala VETA Tanga, Ernest Igobeko, kujiandaa kuanza mafunzo Januari mwakani 2027, ili kuongeza ujuzi wake na baadaye aweze kuwasaidia na kuwafundisha watu wengine wenye mahitaji maalum.
Kasore ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza na Igobeko, katika banda la VETA kwenye Maonesho ya Kitaifa  ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea mkoani Tanga, ambaye ana mahitaji maalum na alikuwa akijifunza ujuzi wa kutengeneza vifaa.
“Jipange, Januari uanze masomo pamoja na mwalimu wako. Serikali itafanya utaratibu wa kukupatia ada kama ilivyo kwa wale walioanza mwaka huu, 2026” amesema.
Amesema mafunzo hayo yatamwezesha Igobeko kujifunza zaidi ya utengenezaji wa vifaa, ikiwamo matumizi ya mashine mbalimbali na kupata utaalamu wa kutengeneza vifaa vinavyoweza kuwasaidia watu wengine wenye mahitaji maalum.
Kasore amesema baada ya kukamilisha mafunzo hayo, Igobeko anaweza pia kupata fursa ya kuwa msaidizi wa mafunzo na kutumia ujuzi atakaoupata kuwafundisha wengine.
Amesema Serikali inaendelea kuweka mazingira yatakayowawezesha watu wenye mahitaji maalum kupata fursa sawa katika elimu na mafunzo ya ufundi, ili waweze kutumia ujuzi wao kujitegemea na kuchangia katika jamii.
Habari Picha 13407
“Usikate tamaa. Kila kitu kinawezekana. Jipange kwa ajili ya mafunzo ili uweze kujifunza vitu vingi zaidi, kujua mashine mbalimbali na hatimaye uweze kuwasaidia wengine,” amesema.
Kwa upande wake, Igobeko amesema mafunzo aliyopata VETA yamemsaidia kuongeza kujiamini na kuonyesha kuwa watu wenye mahitaji maalum wana uwezo wa kufanya kazi za ufundi na kushiriki katika shughuli za maendeleo.
“Nawashukuru na kuwapongeza kwa sababu mmetupa nafasi ya kuonyesha uwezo wetu. Watu wenye mahitaji maalum kama sisi tunaweza kufanya kazi na kuchangia katika jamii badala ya kuwa tegemezi,” amesema.
Amesema mafunzo hayo yamemwezesha kupata ujuzi wa kutengeneza vifaa na kusaidia kubadili mtazamo wa baadhi ya watu waliokuwa wakiamini kuwa mtu mwenye ulemavu hawezi kufanya kazi za ufundi.
Igobeko amesema mafanikio hayo yameleta mabadiliko pia katika familia yake, baada ya kuona kazi anazoweza kufanya, jambo lililompa furaha na kuongeza hamasa ya kuendelea kujifunza.
Amesema anatarajia kutumia mafunzo atakayoanza Januari mwakani 2027 kuongeza ujuzi wa kutumia mashine mbalimbali na baadaye kuwasaidia watu wengine wenye mahitaji maalum kupata ujuzi na kujiamini.
Ametoa wito kwa watu wenye mahitaji maalum kutumia fursa zinazotolewa na Serikali katika mafunzo ya ufundi, akisema ujuzi huo unaweza kuwa msingi wa kujitegemea na kuchangia maendeleo ya jamii.

You Might Also Like

Utunzaji Ziwa Victoria Wasisitizwa kwa Mustakabali wa Uchumi, Mazingira

Wafanyabiashara: Tupo Tayari Kushirikiana na Serikali

Rais Dkt Mwinyi Afika Katika Dua ya Kumuombea Rais Mstaafu Wa Awamu Ya Pili

Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa

Waratibu Wa Kitaifa Wa Nchi Za Jumuiya Ya Ukanda Wa Maziwa Makuu Wakutana Kinshasa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Airtel Yajenga Darasa La Fursa Katika Shule Ya Sekondari Magaoni,Tanga
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Airtel Yajenga Darasa La Fursa Katika Shule Ya Sekondari Magaoni,Tanga
Habari August 23, 2026
Bunifu ya dawa ya mayai yapunguza hasara kwa wafugaji wa kuku
Makala August 22, 2026
Dkt Yonaz Awakumbusha Vijana Kulinda Afya Zao Katika Mapambano Dhidi Ya Ukimwi
Habari August 22, 2026
Maji Yageuka Gesi, Lusano Aibua Ubunifu wa Nishati Safi
Makala August 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?