MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MNH Kuvuna Mifupa Kutengeneza Taya
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > MNH Kuvuna Mifupa Kutengeneza Taya
Habari

MNH Kuvuna Mifupa Kutengeneza Taya

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA:HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH), imeanzisha huduma ya kuvuna mifupa ya mbavu na nyonga kwa ajili ya kutengeneza taya ya chini ambapo gharama yake itakuwa Sh.Milioni 6.2.
Mkurugenzi huduma ya Upasuaji Muhimbili, Dkt.Rachel Mhavile amesema hayo wakati wa kutoa taarifa ya mafanikio kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa Habari Maelezo Jijini Dodoma.
Amesema  huduma hiyo ni mpya katika hospitali za Umma nchini na itasaidia kuimarisha taya ya chini, mifupa hiyo itavunwa kwa mgonjwa mwenyewe baada ya kufanyiwa vipimo na kuona ni jinsi gani inafaa.
Akitoa ufafanuzi juu ya mifupa hiyo amesema kuwa mifupa itavunwa kwa mgonjwa mhusika anayetaka huduma ya kutibiwa taya na pindi atakapokuwa amepatiwa matibabu itakuwa moja kwa moja na siyo ya kutoa na kurejesha.
Pia amesema huduma hiyo itasaidia kutengeneza mizizi bandia ya meno ambayo nayo atawekewa mgonjwa , pia mgonjwa hatapata usumbufu wa kubadilisha mizizi hiyo au taya.
Akizungumzia suala la mafanikio kwa ajili ya watoto wanaozaliwa na tatizo ya kutosikia amesema kuwa Hospitali imeweza kuanzisha huduma ya upasuaji na kuweka vifaa vya kusaidia kusikia.
Amesema kwa sasa watoto 54 wamefanyiwa upasuaji na kuwekewa vifaa vya kuwasaidia kusikia kwa gharama ya Sh.  bilioni 2.3 kwa wote na kusaidia kuokoa kiasi cha shilingi Bilioni nne kama wangeenda kutibiwa nje ya nchi.
Amesema huduma hiyo ya upasuaji kwa watoto ni kati ya watoto wa siku moja hadi miaka mitano ambao uchunguzwa na madakitari bingwa na bobezi ambao ni wazawa.

You Might Also Like

TASU yaiomba serikali inunue kutoa ajira kwa mabaharia

Majukwaa YA Dini Yaimarishe Mapambano Dhidi ya Magonjwa Ya Mlipuko

Walimu Wanaofundisha Lugha Ya Kichina Tanzania Wakutana

Waziri Mkuu Kumwakilisha Dkt Samia Ivory Coast

TARI Yakutanisha Wadau Afya Ya Udongo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article MOI Yaeleza Sababu Viungo Bandia Kuuzwa Kwa Bei Kubwa
Next Article BUWSSA Yapewa Bilioni 28 Kutatua Tatizo La Maji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima
Habari August 7, 2025
Mbegu Bora za Mpunga Zazalishwa TARI Dakawa, Ifakara
Habari August 7, 2025
Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima
Habari August 7, 2025
Mafua, Kifua Yadaiwa Kusababisha Kifo cha Job Ndugai
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?