MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VIONGOZI WA DINI WAONYA: ‘TUMIENI BUSARA, LINDENI AMANI WAKATI WA UCHAGUZI’
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VIONGOZI WA DINI WAONYA: ‘TUMIENI BUSARA, LINDENI AMANI WAKATI WA UCHAGUZI’
Habari

VIONGOZI WA DINI WAONYA: ‘TUMIENI BUSARA, LINDENI AMANI WAKATI WA UCHAGUZI’

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu, 
KILIMANJARO: VIONGOZI wa dini kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga wameibua hoja saba za msingi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu 2025 wakisisitiza amani, haki na busara kwa vyombo vya dola.
Habari Picha 10150
Wakizungumza katika Kongamano la Amani lililofanyika katika ukumbi wa Uhuru Hostel, Moshi, viongozi hao wakiwemo Masheikh, Maaskofu, Mapadri na Wachungaji wametoa wito kwa Watanzania kuendeleza umoja na kuwapuuza wanaohamasisha vurugu.
Katibu wa BAKWATA mkoa wa Kilimanjaro, Alhaji Awadhi Lema, akisoma maazimio ya kongamano hilo, amesema viongozi wa dini wamekubaliana kuhimiza wananchi kuhakiki majina yao na kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani.
Amesema pia wameazimia kuendelea na makongamano ya amani, kuelimisha waumini kuhusu haki na wajibu wao, na kuonya dhidi ya uchochezi mitandaoni.
“Vyombo vya dola vinapaswa kutumia busara na hekima kulinda amani, hasa siku ya uchaguzi,” amesema Lema.
Aidha, viongozi hao walipendekeza viongozi wa dini washirikishwe zaidi katika vyombo vya maamuzi na kutunga sheria, huku wakisisitiza kila raia ana wajibu wa kulinda amani wakati wa kudai haki.
Sheikh wa Mkoa wa Kilimanjaro, Sheikh Shaban Mlewa, amesema Watanzania wanapaswa kujifunza kutoka kwa mataifa yaliyopoteza amani, akisisitiza umuhimu wa uzalendo, upendo na uadilifu.
“Amani ni urithi muhimu, tusiiache ipotee mikononi mwetu,” amesema.
Sheikh wa Mkoa wa Arusha, Sheikh Shaban Juma, ameongeza kuwa haki haiwezi kupatikana bila amani.
“Amani inajengwa kwa kumcha Mungu, kujitambua na kulinda uhai wa wengine,” amesema.
Kwa upande wake, Wakili Mchungaji Daniel Swai wa KKKT Kaskazini amesema ni kosa mtu kuhamasisha wengine kutopiga kura, akisisitiza haki na amani haviwezi kutenganishwa.
Padri Deogratias Matiika wa Jimbo Katoliki la Moshi amewataka wananchi na viongozi kuheshimiana na kuepuka matusi mitandaoni.
“Kuheshimu haki ni msingi wa utulivu wa taifa,” amesema.
Padri Francis Mahimbo wa Kanisa la Anglikana Tanga amewataka Watanzania kuendeleza uvumilivu na kuheshimu haki za binadamu ili taifa liendelee kuwa na amani.
Kongamano hilo pia liliwahusisha kamati za dini za wanawake na vijana, ambazo ziliwataka Watanzania kushiriki uchaguzi kwa amani na kuwakataa wanaotaka kuchochea vurugu au uvunjifu wa sheria.

You Might Also Like

Watanzania Washauriwa Kula Senene, Kumbikumbi, Msusa, Ngogwe Kuepuka Udumavu

Elimu Ya Fedha Yafika Makanya Same

Limeni mkonge unalipa – Maghali

Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi

Rais Samia katika uzinduzi rasmi safari za SGR

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CHAUMMA YAAPA KUJENGA BUNGE LA WABUNGE WA HOJA, SI MACHAWA
Next Article MWALIM AOMBA WATANZANIA KUMWOMBEA WIKI YA MWISHO KUELEKEA UCHAGUZI
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Diwani Kata Ya Majengo Awasihi Wananchi Kufanya Kazi Kwa Bidii
Habari February 16, 2026
Tanzania Yalenga Kufikia Asilimia 51 Ya Ushiriki Wa Wanawake Katika Sayansi
Habari February 14, 2026
Makamu wa Rais Asisitiza Ubunifu, Uwekezaji Soko La Hisa La Dar es Salaam
Habari February 13, 2026
JAB Yasisitiza Ithibati Kama Njia ya Kuimarisha Ubora na Uaminifu wa Habari
Habari February 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?