MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Miradi Ya Kusambaza Umeme Vitongojini Kukamilika Ifikapo 2030
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Miradi Ya Kusambaza Umeme Vitongojini Kukamilika Ifikapo 2030
Habari

Miradi Ya Kusambaza Umeme Vitongojini Kukamilika Ifikapo 2030

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI  imeeleza mafanikio makubwa ya utekelezaji  wa miradi ya kusambaza umeme maeneo ya vijijini  na pembezoni mwa miji ambapo  kupitia Wakala wa Nishati Vijijini  (REA) imefanikiwa kufikisha huduma ya umeme kwenye vijiji vyote 12,318.

Hatua hiyo ni sawa na asilimia 100 ya miradi ya umeme kwenye vitongoji inatarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2030.

Mafanikio ya miradi ya umeme Vijijini  yamebainishwa leo Oktoba 8, 2025 na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Umeme Vijijini  Jones Olotu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa Wiki ya Huduma kwa Wateja jijini Dodoma.

“Tanzania bara tuna jumla ya vitongoji 64,359 ambapo kati ya hivyo vitongoji  37,328 sawa na asilimia 58 vimeshafikiwa na huduma ya umeme na bado miradi ya kusambaza na kufikisha huduma ya umeme inaendelea katika maeneo mbalimbali nchini,” Amesema Olotu.

Halikadhalika, Olotu ameongeza kuwa, Wakala wa Nishati Vijijini unatarajia kukamilisha utekelezaji wa kusambaza umeme kwenye maeneo ya vitongoji ifikapo mwaka 2030 ili watanzania wapate huduma ya umeme ili kukuza maendeleo yao binafsi na uchumi wa Taifa.

Katika hatua nyingine,  Olotu amesema Serikali imepata watoa huduma kwa ajili ya kufungwa mifumo ya umeme jua kwa wakazi wa maeneo ya visiwani Tanzania bara ipatayo 20,000.

Katika hatua nyingine,  Olotu amewaasa wananchi kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali kupitia REA hususan nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kujikinga na madhara ya kiafya,  kimazingira na kiuchumi yanayotokana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama.

Vilevile, Serikali kupitia REA inaendelea kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta maeneo ya vijijini ili wananchi waweze kuhifadhi salama bidhaa za mafuta.

Watumishi wa REA wameipamba Wiki ya Huduma kwa Wateja ambayo inafanyika katika ofisi ya Wakala wa Nishati Vijijini makao Makuu jijini Dodoma.

 

You Might Also Like

Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta

Taasisi Za Dini Zinazofanya Biashara Zinatakiwa Kulipa Kodi

UDSM Yaja Na Bajaji Inayotumia Maji Na Mafuta

FCC Yatatua Kero 63  Za Walaji

Maboresho Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Uwekezaji Kuchochea Uwekezaji Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wizara Ya Nishati Yaendelea Kutoa Elimu Kuhusu Matumizi Ya Nishati Safi Ya  Kupikia
Next Article Asisitiza Umuhimu Wa Kukamilisha Miradi Kwa Mujibu Kuzingatia Mikataba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Habari March 12, 2026
Mamlaka Za Mitaa Ondoeni Urasimu Katika Kuanzisha Biashara Mpya-Waziri Mkuu
Habari March 12, 2026
Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani
Habari March 12, 2026
GCLA  Yanunua Mitambo Mikubwa Inayogharimu Sh Bil 32.25 Kuimarisha Uchunguzi Wa Sampuli
Habari March 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?