MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini
Habari

Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
MGOMBEA Ubunge Jimbo la Dodoma Mjini kupitia CCM, Samwel Malecela, ameahidi atatoa kipaumbele kwa vijana kwa kuanzisha shule maalum ya kuibua vipaji kuanzia utotoni.
 Akizungumza na wajumbe wa CCM katika Kata ya Mpunguzi, Malecela amesema vipaji vimekuwa chanzo kikubwa cha ajira kwa vijana duniani kote, hivyo kuvitambua na kuviendeleza mapema ni njia sahihi ya kuwawezesha kiuchumi.
Amesema shule hiyo itakuwa kichocheo cha kuongeza kipato kwa vijana na kuchangia pato la jimbo zima.
“Leo hii vipaji ni ajira, na iwapo watoto wetu wataandaliwa mapema, watakuwa na nafasi kubwa ya kufanikiwa kuliko kusubiri hadi mtu awe mtu mzima,” amesema.
Sambamba na hilo, ameahidi kushughulikia upatikanaji wa mikopo ya halmashauri kwa wakati kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Amesema akiwa mbunge, atatumia nafasi yake kushinikiza utoaji wa mikopo hiyo usicheleweshwe, kwani ni haki yao kwa mujibu wa sera za serikali.
Aidha, Malecela alizungumzia mpango wa kuvutia wawekezaji hasa katika kata ya Matumbulu, ili kuongeza ajira na kukuza uchumi wa maeneo hayo.
Amesema pia changamoto ya maji kama moja ya kipaumbele atakachoshughulikia kwa kushirikiana na serikali kupitia utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Vile vile amesema Katika kata ya Mkonze, Samwel Malecela amekemea vikali vitendo vya upotevu wa mali za umma na migogoro ya ardhi vinavyoathiri maendeleo ya wananchi.
Akijibu maswali ya wajumbe wa CCM katika kata hiyo, amesema hatakubali wananchi kuendelea kunyimwa maendeleo kwa sababu ya ubadhirifu wa wachache.
“Baadhi ya watumishi wamekuwa wakihusika na ufisadi wa mali za umma huku wananchi wakibaki masikini.
“Hili ni jambo nitakalokomesha nikiwa mbunge,” amesema.
Pia aliahidi kushughulikia kero ya barabara kwa kuhakikisha zinajengwa kwa kiwango cha changarawe ili ziweze kupitika kwa urahisi.

You Might Also Like

Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko

Timu Wizara Ya Nishati Zawasili Tayari Kwa Bonanza

TUCTA Yakutana Na Mkuu Wa Mkoa Mbeya, Maandalizi Mei Mosi kitaifa 2025.

TPHPA yakusanya zaidi ya sampuli 10,000 za mbegu asili

Rais Samia Azungumzia Mafanikio Ya Nishati Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini
Next Article Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Habari August 1, 2025
Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Habari August 1, 2025
Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Habari August 1, 2025
Njaa, Mafao Ya Wakulima Vyatikisa Kampeni Za Ubunge Dodoma Mjini
Habari July 31, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?