MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu
Habari

Watafiti Watumia Mbinu Mpya Kudhibiti Mdudu Kantangaze Kwenye Nyanya Bila Viuatilifu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WATAFITI kutoka Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa mkoani Iringa, wamefanikiwa kuibua mbinu mpya ya kudhibiti mdudu kantangaze ambaye ni adui mkubwa wa zao la nyanya kwa kutumia njia isiyo ya kemikali.

Mhadhiri Mwandamizi wa Kemia chuoni hapo, Dkt. Juma Mmongonyo ameeleza hayo alipozungumza na Mwandishi wa Mfanyakazi katika Banda la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Mhadhiri huyo amesema wakiwa kama timu wameweza kufanya utafiti na kufanikiwa kwa asilimia kubwa
kumdhibiti mdudu huyo, ambaye amekuwa tatizo kubwa kwa wakulima wa nyanya nchini.

Amesema mdudu kantangaze husababisha hasara kubwa kwa wakulima, kiasi cha kulazimika kutumia viuatilifu kila wiki kwa muda wa hadi miezi sita ili kuokoa mazao yao.

Amesema hali hiyo si tu inawagharimu wakulima fedha nyingi, bali pia ina athari za kiafya kwa walaji kwa kuwa mabaki ya viuatilifu hubakia kwenye nyanya, pamoja na uharibifu wa mazingira.

Amesema katika utafiti huo uliofanyika Iringa kwa kushirikiana na wakulima mashambani, watafiti wamegundua dawa mbadala iitwayo SPLAT yenye uwezo mkubwa wa kumdhibiti mdudu kantangaze kwa kutumia mfumo wa kuvutia na kuua madume ya mdudu huyo.

Kwa mujibu wa Dkt. Mmongoyo, dawa hiyo ina harufu inayofanana na ile ya kantangaze jike, hivyo humvutia dume ambaye huja akidhani amepata mwenza, lakini badala yake huangamia.

“Kwa njia hii, tunakata mzunguko wa uzalishaji wa wadudu, kwani madume yanapokosekana, majike hayatapata wenza wa kuzaliana nao,” amesema.

Amesema matokeo ya awali yanaonesha kuwa matumizi ya SPLAT huweza kupunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya kantangaze mashambani ndani ya kipindi cha wiki tatu, ikilinganishwa na utumiaji wa viuatilifu kila wiki kwa miezi sita.

Amesema mbinu hiyo si tu inawalinda walaji dhidi ya mabaki ya sumu kwenye vyakula bali pia inampunguzia mkulima mzigo wa gharama za kununua dawa kila wiki.

Aidha, inahakikisha nyanya zinazozalishwa zinakuwa safi na bora zaidi, na hivyo zina nafasi ya kukubalika kwenye soko la kimataifa linalohitaji viwango vya juu vya usalama wa chakula.

“Tulianza kufuatilia matokeo ya matumizi ya dawa hii Januari hadi sasa Julai, na tumefurahishwa sana na mafanikio yake.

“Tumeanza maandalizi ya awamu ya pili ya utafiti kwa kipindi cha kiangazi,” amesema.

You Might Also Like

Kongani za viwanda kutoa ajira nchini.

Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria Yasisitiza Uhifadhi

Serikali  Kuja Na Mradi  Wa Kuimarisha Upatikanaji Umeme Vitongojini- Kapinga 

Mbunge wa Monduli Aahidi Kusimamia Changamoto za Jimbo Lake

Diwani Kata Ya Majengo Awasihi Wananchi Kufanya Kazi Kwa Bidii

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article PSSSF Itaendelea Kuwekeza Kwenye Maeneo Salama Yenye Tija
Next Article MAIPAC Yagawa Makoti Ya Usalama Kwa Wanahabari Kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ziwa Ngozi Lavuta Mamia Sabasaba, Wageni Washangazwa Na Ramani Ya Afrika Juu Ya Mlima
Habari July 9, 2026
Shirika La Uzalishaji Mali La Polisi Kujenga Vituo Vya Ukaguzi Wa Vyombo Vya Moto
Habari July 9, 2026
Watumishi 7881 Watakaostaafu 2026/27 Watambuliwa Kupitia Kampeni Ya Tunalipa Jana-PSSF
Uncategorized July 8, 2026
Katambi Apongeza Zimamoto Kwa Uwekezaji Wa Vifaa Vya Kisasa
Uncategorized July 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?