MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Makamu Mkuu OUT: Elimu ya Masafa Yahitaji Nidhamu ya Hali ya Juu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Makamu Mkuu OUT: Elimu ya Masafa Yahitaji Nidhamu ya Hali ya Juu
Habari

Makamu Mkuu OUT: Elimu ya Masafa Yahitaji Nidhamu ya Hali ya Juu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DODOMA: WANAFUNZI wapya na wanaoendelea wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wametakiwa kuwajibika katika masomo, kuwa na nidhamu ili kuhitimu kwa wakati.
Makamu Mkuu wa OUT, Profesa Alex Makulilo, amesema hayo katika hotuba yake ya ukaribisho kwa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2025/2026.
Amesema wanafunzi wanapaswa kuwa makini na masomo yao na kufuatilia programu za ufundishaji, hususan mihadhara ya mtandaoni kupitia programu tumizi ya Zoom.
Habari Picha 10351
“Napenda kuwakumbusha kwamba kusoma Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kunahitaji nidhamu binafsi na kujituma,” amesema Profesa Makulilo.
Aidha, amesema chuo kitaendelea kutoa ratiba za ufundishaji mara kwa mara ili wanafunzi wafuatilie masomo bila kuachwa nyuma.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kituo cha Mkoa cha OUT – Dodoma, Dkt. Mohamed Msoroka, amesema kusoma kwa mafanikio kunawezekana kwa kila mtu, hasa kwa wale wanaojituma na kutumia muda wao vizuri.
Habari Picha 10352
Amesisitiza wanafunzi kujihusisha kikamilifu katika vipindi na mihadhara ya mtandaoni pamoja na ile ya ana kwa ana, na kutafuta msaada wanapouhitaji.
Amesema kwa kuwa wadahiliwa wengi ni watu wazima wenye familia, ajira na majukumu mengine, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilianzishwa ili kuwapa urahisi, uhuru na fursa ya kuendelea na elimu ya juu bila kuathiri majukumu yao.
“Mafanikio katika ujifunzaji kwa njia ya elimu huria na ya masafa yanahitaji nidhamu binafsi, kujitolea na uwezo mzuri wa kusimamia muda,” amesema Dkt. Msoroka.
Mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Kituo cha Mkoa cha Dodoma, Sabina Mpigauzi, anayesomea ualimu, ametoa wito kwa watumishi wa umma na sekta binafsi kujiendeleza kitaaluma kupitia Chuo hicho kwani kinawawezesha kuendelea na masomo bila kuathiri majukumu yao mengine kama ajira, malezi na uangalizi wa familia.

You Might Also Like

JOWUTA Yakutana na Waziri Ridhiwani, Kamishna wa Kazi Kujadili Changamoto za Wanahabari

TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea

Miradi Ya Kusambaza Umeme Vitongojini Kukamilika Ifikapo 2030

Serikali yatambua deni la Kiwira Coal Mine Bill.1.52

PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article ADA-TADEA Yamsimamisha Uanachama Mgombea Mwenza, Yajaza Nafasi Zilizo Wazi
Next Article Simbachawene: Nitaheshimu Mfumo Wa Uongozi Na Kushirikiana
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchi za SADC Zahimizwa Kuimarisha Umoja Kukabili Changamoto
Uncategorized July 17, 2026
Wananchi Washauriwa Kutumia  Wataalam Wa Ujenzi Kuepuka Madhara
Habari July 14, 2026
July 14, 2026
Uncategorized July 14, 2026
TANESCO Kutambulisha Mfumo Wa Kufunga Nyaya Kwenye Nyumba Ukifuatilia Matumizi Ya Umeme
Habari July 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?