MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kundi Kubwa La Wanafunzi Hukatisha Masomo Katika Ngazi Mbalimbali Ya Elimu -TEWW 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kundi Kubwa La Wanafunzi Hukatisha Masomo Katika Ngazi Mbalimbali Ya Elimu -TEWW 
Habari

Kundi Kubwa La Wanafunzi Hukatisha Masomo Katika Ngazi Mbalimbali Ya Elimu -TEWW 

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu, Dodoma
TAASIS  ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) imesema  takwimu zinaonyesha  katika   kila watoto 10 kwa baadhi ya maeneo, wanne  kati yao hawapati fursa ya kuanza shule, huku kundi kubwa la wanafunzi likikatisha masomo katika ngazi mbalimbali za elimu.
Hata hivyo   imesema inaendelea  kuwawezesha watoto, vijana na watu wazima waliokosa fursa ya elimu ndani ya mfumo rasmi kurejea na kuendelea na masomo yao.
Mkuu wa Taasisi hiyo, Profesa Philipo Sanga,  amesema katika wakati Wiki ya utumishi wa Umma katika viwanja vya Chinangali Park Mkoani Dodoma.
Amesema majukumu makubwa ya TEWW ni kushughulikia elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi, sekta ambayo imekuwa muhimu katika kuwasaidia wananchi wengi kupata elimu na ujuzi unaohitajika katika maisha na maendeleo ya taifa.
“Katika kila wanafunzi 100, takribani 31 hudondoka na kushindwa kuendelea na masomo kwa ujumla, zaidi ya wanafunzi laki nne kutoka shule za msingi na sekondari hudondoka kila mwaka na kukosa fursa ya kuendelea na elimu.”
Amebainisha kuwa bila uwepo wa Taasis ya Elimu ya Watu Wazima, idadi kubwa ya wananchi wengi wangeshindwa kupata nafasi ya kurejea katika mfumo wa elimu na kufikia malengo yao.
Profesa Sanga,  amesema Taasisi hiyo inatekeleza miradi mbalimbali ya elimu ya msingi na sekondari nje ya mfumo rasmi, inayolenga kuwapa wananchi fursa ya kupata elimu, maarifa na ujuzi unaowawezesha kujitegemea na kuchangia maendeleo ya taifa.
Aidha, amesema TEWW kupitia Chuo cha Elimu ya Juu cha Elimu ya Watu Wazima hutoa programu za elimu kuanzia ngazi ya cheti, stashahada, shahada hadi shahada za uzamivu kwa lengo la kuandaa wataalamu wabobevu watakaosaidia maendeleo ya nchi.
Ameongeza kuwa katika kila mkoa kuna viongozi wa elimu ya watu wazima wanaosimamia shughuli za taasisi hiyo na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi katika maeneo mbalimbali.
Kuhusu elimu ya juu, Profesa Sanga amesema Taasis ya Elimu ya Watu Wazima imefanikiwa kudahili zaidi ya wanafunzi 6,000 na kwamba zaidi ya wanafunzi 2,000 huhitimu kila mwaka, jambo linaloonyesha mchango mkubwa wa taasisi hiyo katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

You Might Also Like

JOWUTA Yawasilisha Ripoti ya Ukaguzi kwa Msajili

TARURA Yaimarisha Upitikaji Miundombinu Ya Barabara

Katoro Yapata Gari Jipya la Zimamoto, Kuwasili Februari 9

COSTECH, CRDB Foundation Yazindua Mikopo Nafuu Kwa Wabunifu

Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TEMESA  Yajadhimisha Miaka 20, Yajivunia  Mafanikio  Na Kuahidi  Kuimarisha  Huduma
Next Article VETA  Yapongezwa Kwa Kuibua Vipaji Kwa Vijana  
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA  Yapongezwa Kwa Kuibua Vipaji Kwa Vijana  
Habari June 24, 2026
TEMESA  Yajadhimisha Miaka 20, Yajivunia  Mafanikio  Na Kuahidi  Kuimarisha  Huduma
Habari June 24, 2026
PURA Yasema Tanzania Inaendelea Kujivunia Uwepo Wa Gesi Asilia,Ni Nguzo Muhimu Katika Kuchochea Maendeleo
Habari June 24, 2026
TMA Yatoa Elimu ya Hali ya Hewa kwa Wananchi Dodoma
Habari June 23, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?