MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Walimu Ni Nguzo ya Maadili na Uzalendo kwa Taifa – Rais CWT
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Walimu Ni Nguzo ya Maadili na Uzalendo kwa Taifa – Rais CWT
Habari

Walimu Ni Nguzo ya Maadili na Uzalendo kwa Taifa – Rais CWT

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Dkt. Suleiman Ikomba, amesema kuwa nafasi ya mwalimu haijikiti tu kwenye kufundisha darasani, bali pia inahusisha kulea maadili, kujenga uzalendo na kuwa kielelezo bora kwa kizazi kijacho.
Akizungumza katika mahojiano maalum, Dkt. Ikomba ameeleza kuwa jukumu la mwalimu linazidi mipaka ya maandalizi ya masomo, kwani linahusisha kujenga jamii yenye nidhamu, utu na uwajibikaji.
Akizungumzia mchango wa CWT, amesema chama hicho kinaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha walimu wanadumisha hadhi ya kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.
Amefafanua kuwa, chama kinaweka mkazo katika kuimarisha maadili ya taaluma ya ualimu kupitia mikutano, semina na majadiliano ya kitaaluma kwa wanachama wake, ili kuwakumbusha wajibu wao kwa wanafunzi, jamii na taifa.
Aidha, amebainisha kuwa CWT inashirikiana na mamlaka husika kukuza taaluma ya walimu, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wao katika kufundisha na kulea kwa weledi zaidi.
Pia amesisitiza umuhimu wa walimu kuzingatia uwajibikaji na nidhamu ya kazi, akieleza kuwa mwalimu mwenye maadili na ujuzi wa hali ya juu huwa kielelezo cha jamii nzima.
Dkt. Ikomba amehitimisha kwa kusisitiza kuwa lengo kuu la chama hicho ni kuhakikisha mwalimu wa Tanzania anapata heshima stahiki, anawajibika ipasavyo na anakuwa mfano bora kwa wanafunzi pamoja na jamii kwa ujumla.

You Might Also Like

Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana

Shemdoe aridhika huduma zinazotolewa na TVLA nanenane

Rais Samia Ni Mama Wa Maendeleo – Majaliwa

Mbunge Ulanga Aweka Mikakati Kuufungua Mkoa wa Morogoro Kimaendeleo

Majaliwa Asisitiza Serikali Itaendelea Kuboresha Mazingira Ya Uwekezaji

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Uwekezaji wa NSSF wa Mzizima Towers Kufungua Fursa Mpya za Biashara na Utalii Dar
Next Article Upotevu Wa Maji Kipimo Cha Utendaji Wa Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

IITA Yawekeza Bilioni 410 Tanzania Kuimarisha Kilimo, Utafiti
Habari May 9, 2026
Vyuo Vikuu Vyahitaji Mkakati Madhubuti wa Tafiti — Yanda
Habari May 8, 2026
Asilimia 26 Ya Wanawake Ndio Wanaoamini Kuwa Na Uhuru Wa Kufanya Maamuzi Ya Kufanya Shughuli Za Uchumi
Habari May 8, 2026
Kesi 100 Za Wananchi Zasikilizwa Na Kupatiwa Suluhu Katiba Na Sheria
Habari May 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?