MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: NIC Yaimarisha Uhusiano na Wateja Maonesho ya Teknolojia ya Madini Geita
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > NIC Yaimarisha Uhusiano na Wateja Maonesho ya Teknolojia ya Madini Geita
Habari

NIC Yaimarisha Uhusiano na Wateja Maonesho ya Teknolojia ya Madini Geita

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
GEITA: SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC) limeshiriki katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini, yanayoendelea mkoani Geita, kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kuongeza ukaribu na wateja wake.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa NIC, Karimu Meshack, amefanya ziara ya kutembelea mabanda ya taasisi mbalimbali za kifedha, bima na sekta ya madini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za taasisi hiyo kushirikiana kwa karibu na wadau wake.
Habari Picha 9655
Miongoni mwa taasisi alizotembelea ni pamoja na Benki ya NMB, Benki ya Equity, Bluecoast, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Sekta Binafsi (NSSF), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Kampuni ya Madini ya FEMA, pamoja na Wakala wa Bima wa HEXAD.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo katika banda la Benki ya NMB,  Meshack amesema,
Habari Picha 9656
“Tumekuja kuwashukuru kwa kuendelea kutumia huduma za NIC. Pia tunalenga kuimarisha ushirikiano wetu wa kibiashara, kutambua changamoto zilizopo na kuhakikisha tunazitatua kwa wakati.”
Maonesho hayo ambayo hufanyika kila mwaka, yanawakutanisha wadau kutoka sekta ya madini, teknolojia, fedha, na bima, huku kwa mwaka huu yamefunguliwa rasmi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Habari Picha 9657
NIC imeendelea kutoa huduma na elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa bima katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
 Wananchi wanakaribishwa kutembelea banda la NIC lililopo karibu na mabanda ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Chuo cha Teknolojia ya Madini (TTC), kwa ajili ya kupata huduma za bima, ushauri wa kitaalamu na maelezo ya kina kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za shirika hilo.
Habari Picha 9658
Habari Picha 9659

You Might Also Like

DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa

VIONGOZI WA DINI WAONYA: ‘TUMIENI BUSARA, LINDENI AMANI WAKATI WA UCHAGUZI’

OCMS Kuleta Usawa na Haki Kwa Wafanyakazi

WCF Yatakiwa Kuongeza Nguvu Kusajili Waajiri

UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TFS Yashiriki Maonesho ya Nane ya Madini Geita
Next Article NIC Yatoa Elimu ya Bima Kwenye Kijiji cha Bima, Maonesho ya Madini Geita
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Habari December 5, 2025
DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Habari December 5, 2025
Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Habari December 4, 2025
Profesa Silayo Aaga, Jawara Kuchukua Uongozi Mpya wa AFWC25
Habari December 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?