MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Watendaji Wakuu Waagizwa Kuifanya Dira 2050 Kuwa Mwongozo Wa Maamuzi Yao
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Watendaji Wakuu Waagizwa Kuifanya Dira 2050 Kuwa Mwongozo Wa Maamuzi Yao
Habari

Watendaji Wakuu Waagizwa Kuifanya Dira 2050 Kuwa Mwongozo Wa Maamuzi Yao

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
WATENDAJI Wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali wameagizwa kuhakikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inakuwa msingi wa maamuzi, mipango na bajeti za taasisi wanazoziongoza ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.
Agizo hilo limetolewa Julai 24, 2026 mjini Kibaha, mkoani Pwani, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma yaliyolenga kuimarisha uongozi na utendaji.
Ridhiwani amesema kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ulianza rasmi Julai Mosi mwaka huu 2026, hivyo kila taasisi inapaswa kuoanisha mipango yake ya kimkakati, bajeti na vipaumbele na malengo ya dira hiyo.
Habari Picha 12889
Amesisitiza kuwa mafanikio ya Dira 2050 hayatapatikana kwa matamko pekee, bali kupitia maamuzi ya kila siku ya viongozi wa taasisi za umma.
Amesema kila bajeti, mradi, uwekezaji na huduma inayotolewa inapaswa kuonyesha mchango wake katika kufanikisha malengo ya dira hiyo.
Pia amewataka Watendaji Wakuu kuhakikisha viashiria vya utendaji vya taasisi zao vinaendana na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ili kurahisisha upimaji wa mchango wa kila taasisi katika utekelezaji wake na kuimarisha uwajibikaji.
Habari Picha 12890
“Nina imani kuwa maarifa na uzoefu mlioupata utatafsiriwa katika utendaji wenye matokeo chanya, hivyo kuimarisha utawala bora, kuongeza ufanisi wa Taasisi za Umma na kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwa manufaa ya maendeleo endelevu ya Taifa,” amesema Ridhiwani.
Ridhiwani aliipongeza Ofisi ya Msajili wa Hazina, Taasisi ya Uongozi na wadau mbalimbali kwa maandalizi na uratibu wa mafunzo hayo, akisema yamewajengea uwezo Watendaji Wakuu kuongoza taasisi kwa ufanisi, kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi na kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya Serikali.

You Might Also Like

Tume Ya Madini Yaweka Vipaumbele Kuwezesha Vijana Kushiriki Katika Uchimbaji Madini 

OUT Yazindua Programu Mpya za Masomo Kukidhi Mahitaji ya Uchumi wa Kisasa

Chagueni Viongozi Wanaofaa-Biteko

Programu Mpya ya TPHPA Yalenga Usalama wa Mazao Sokoni

TPDC na PURA Hakikisheni Watanzania Wananufaika na Rasilimali za Mafuta na Gesi- Salome

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Nchi za SADC Zahimizwa Kuimarisha Umoja Kukabili Changamoto
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchi za SADC Zahimizwa Kuimarisha Umoja Kukabili Changamoto
Uncategorized July 17, 2026
Wananchi Washauriwa Kutumia  Wataalam Wa Ujenzi Kuepuka Madhara
Habari July 14, 2026
July 14, 2026
Uncategorized July 14, 2026
TANESCO Kutambulisha Mfumo Wa Kufunga Nyaya Kwenye Nyumba Ukifuatilia Matumizi Ya Umeme
Habari July 13, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?