MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: PURA Yasema Tanzania Inaendelea Kujivunia Uwepo Wa Gesi Asilia,Ni Nguzo Muhimu Katika Kuchochea Maendeleo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > PURA Yasema Tanzania Inaendelea Kujivunia Uwepo Wa Gesi Asilia,Ni Nguzo Muhimu Katika Kuchochea Maendeleo
Habari

PURA Yasema Tanzania Inaendelea Kujivunia Uwepo Wa Gesi Asilia,Ni Nguzo Muhimu Katika Kuchochea Maendeleo

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu, Dodoma

MAMLAKA Ya Udhibiti Mkondo Wa Juu Wa Petroli (PURA) Tanzania imeanza shughuli ya kutafuta mafuta tangu mwaka 1950 na imechimba visima zaidi ya 97, lakini bado nchi haijafanikiwa kupata mafuta ya kibiashara, lakini imefanikiwa kugundua gesi asilia ambayo inaendelea kutumika katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Mhandisi Charles Sangweni amesema kuwa Tanzania inaendelea kujivunia uwepo wa akiba kubwa ya gesi asilia ambayo imekuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya sekta ya nishati na uchumi wa taifa.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Jijini Dodoma, Sangweni amesema kuwa PURA imeendelea kusimamia shughuli za utafutaji, uchimbaji na maendeleo ya rasilimali za mafuta na gesi kwa mujibu wa sheria na miongozo ya nchi.

Aidha, amebainisha kuwa matumizi ya gesi asilia yanaendelea kuongezeka duniani kutokana na mabadiliko ya teknolojia na juhudi za kupunguza matumizi ya nishati zinazochafua mazingira, hali inayofanya rasilimali hiyo kuwa na umuhimu mkubwa kwa Tanzania.

Ameongeza kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, jambo linaloongeza mahitaji ya gesi asilia na kutoa fursa zaidi za uwekezaji katika sekta hiyo.

Sangweni amesema kuwa PURA imeendelea kuhakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali za petroli kupitia ajira, utoaji wa huduma na bidhaa pamoja na ushirikishwaji katika miradi mbalimbali chini ya sera ya Local Content.

Aidha, amebainisha kuwa mamlaka hiyo imeanzisha mifumo ya kuwaunganisha wataalamu wa Kitanzania na wawekezaji ili kuongeza ajira na kukuza uwezo wa wazawa kushiriki kikamilifu katika sekta ya mafuta na gesi.

Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya utafutaji wa mafuta na gesi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Eyasi Wembere pamoja na vitalu vya Lindi na Mtwara vinavyotekelezwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Kuhusu changamoto za mabadiliko ya bei ya mafuta duniani, Sangweni amesema kuwa Tanzania imeendelea kuwa katika hali nzuri ya upatikanaji wa mafuta licha ya migogoro ya kimataifa inayotokea katika baadhi ya maeneo ya dunia.

Amebainisha kuwa nchi za Afrika Mashariki na Kati zimeendelea kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika matumizi na usambazaji wa rasilimali za nishati ili kuhakikisha usalama wa nishati kwa wananchi hata wakati wa changamoto za kimataifa.

Amesema Afrika inapaswa kuendelea kutumia rasilimali zake za mafuta, gesi na madini kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake huku ikiendelea kuzingatia masuala ya utunzaji wa mazingira.

You Might Also Like

‎ ‎EWURA  Yatoa  Leseni Za Mafundi Umeme  Zaidi Ya 1000

Samia Aendeleza Kampeni Mwanza, Azungumza na Wananchi Misungwi

Tanzania, Ufini Kushirikiana Teknolojia Za Kisasa Sekta ya Misitu

Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa

Sheria Ya Kupata  Taarifa, Ya NGOs Zina Upungufu 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TMA Yatoa Elimu ya Hali ya Hewa kwa Wananchi Dodoma
Next Article TEMESA  Yajadhimisha Miaka 20, Yajivunia  Mafanikio  Na Kuahidi  Kuimarisha  Huduma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA  Yapongezwa Kwa Kuibua Vipaji Kwa Vijana  
Habari June 24, 2026
Kundi Kubwa La Wanafunzi Hukatisha Masomo Katika Ngazi Mbalimbali Ya Elimu -TEWW 
Habari June 24, 2026
TEMESA  Yajadhimisha Miaka 20, Yajivunia  Mafanikio  Na Kuahidi  Kuimarisha  Huduma
Habari June 24, 2026
TMA Yatoa Elimu ya Hali ya Hewa kwa Wananchi Dodoma
Habari June 23, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?