MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari

TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imesema ina jukumu muhimu katika kusaidia kudhibiti magugu vamizi katika Ziwa Victoria kupitia matumizi ya njia za kibaiolojia kwa kutumia wadudu aina ya mbawakavu wanaokula gugu hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Meneja wa TPHPA Kanda ya Ziwa, Juma Mwinyimkuu, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi wakati wa Maonesho ya Kwanza ya Ziwa Victoria.

Amesema TPHPA imeshiriki maonesho hayo kutokana na wajibu wake wa kudhibiti magugu vamizi katika Ziwa Victoria, hususan gugu la Kariba ambalo mwaka jana liliongezeka kwa kasi na kusababisha changamoto kubwa katika ziwa hilo.

Mwinyimkuu amesema taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali katika juhudi za kuondoa gugu hilo.

Aidha, mwishoni mwa mwaka jana 2025, timu ya wataalamu kutoka taasisi mbalimbali ilisafiri kwenda Uganda kujifunza namna nchi hiyo inavyodhibiti gugu hilo kwa kutumia mbinu za kibaiolojia.

Amesema baada ya mafunzo hayo, walirejea na wadudu aina ya mbawakavu wanaoshambulia gugu hilo na kukabidhiwa TPHPA kwa ajili ya kuendelea kuwazalisha.

“Hadi sasa tumefanikiwa kuzalisha zaidi ya wadudu 40,000. Baada ya kujiridhisha kuwa hawana madhara kwa mazingira, tuliwaweka katika maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria kwa ajili ya kupima ufanisi wao,” amesema Mwinyimkuu.

Ameeleza kuwa hatua inayofuata ni kuanzisha eneo maalumu la kuzalisha wadudu hao kwa wingi katika ukanda wa ziwa kabla ya kuwaachia rasmi ndani ya ziwa kwa ajili ya kudhibiti gugu hilo.

Mwinyimkuu amesema mafanikio ya mpango huo yanategemea ushirikiano wa wadau mbalimbali, hivyo TPHPA inaendelea kuwakaribisha taasisi na wananchi kushiriki katika utoaji wa elimu na ujenzi wa uwezo kwa jamii zinazozunguka Ziwa Victoria.

Amesema lengo ni kuunda vikundi vitakavyoshiriki kuzalisha wadudu hao na baadaye kuwaachia katika ziwa ili kusaidia kudhibiti kuenea kwa gugu la Kariba.

You Might Also Like

Mgombea Urais NCCR-Mageuzi Atoa Wito kwa Wananchi Kujitokeza Kupiga Kura

Balozi wa Tanzania Nchini Italy Afurahishwa  Ubunifu wa TPHPA Maonesho ya Nanenane

Serikali Kusaini Muongozo Wa Kima Cha Chini Cha Mshahara Kwa Sekta Binafsi

TUICO Arusha Yapongezwa Na AUWSA

CCM Kuwezesha Wananchi Kufuatilia Mkutano Mkuu Maeneo Ya Wazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Habari May 22, 2026
Biashara 15 Hazitakiwi Kufanywa Na Wageni Ndani Ya Nchi
Habari May 22, 2026
Wadau wataka mifumo jumuishi kupunguza mzigo wa malezi kwa wenye ulemavu
Habari May 21, 2026
Wabunge Waitaka Ujenzi Kuwa Na Mageuzi Makubwa Ya Ujenzi Wa Barabara
Habari May 21, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?