Na Lucy Lyatuu
KATIKA mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imeweka mikakati 30 ya kimkakati inayolenga kuimarisha sekta ya kilimo nchini huku ikidhamiria kuongeza uzalishaji wa zao la miwa kutoka Tano 4351673.1 hadi tani 5500,000.
Aidha Wizara hiyo imeomba kuidhinishiwa trilioni 1,105,950,115 jambo litakalowezesha kuongeza tija na uzalishaji, kuchochea ajira kwa vijana na wanawake, pamoja na kuimarisha usalama wa chakula na lishe kwa wananchi.
Waziri wa Kilimo,Daniel Chongolo amesema hayo bungeni Dodoma na Waziri wa Kilimo, wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Kuhusu mikakati hiyo, Chongolo amesema Wizara imejipanga kutekeleza mikakati hiyo katika maeneo manne makuu yanayolenga kubadili taswira ya sekta ya kilimo nchini.
Kuhusu zao la miwa na uzalishaji wa sukari amesema tani 4351673.1 zilizozalisha sukari tani 410979…04 mwaka 2025/26 hadi tani 5500,000 za miwa zitakazozalisha sukari tani 550,000.
Amesema vile vile Wizara kupitia TARI itaanzisha shamba la kuzalisha mbegu za miwa Lenye ukubwa wa ekari 10 katika Halmashauri ya Kilosa ambalo litakuwa na uwezo wa kuzalisha jumla ya tani 400 za mbegu za miwa.
Kuhusu kuongeza tija na uzalishaji, Serikali imeelekeza nguvu katika utafiti wa kilimo, uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora na miche, pamoja na utoaji wa ruzuku ya mbolea, mbegu na viuatilifu kwa wakulima.
“Mikakati mingine ni pamoja na usajili wa wakulima, kuimarisha huduma za ugani, kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja na kupima afya ya udongo, pamoja na kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na vituo vya huduma za zana za kilimo,”amesema.
Kuhusu kuhakikisha usalama wa chakula na lishe nchini, Serikali imepanga kuwekeza katika miundombinu ya uhifadhi wa chakula ili kufikia uwezo wa kuhifadhi tani milioni 3 ifikapo mwaka 2030. Aidha, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) utaongezewa uwezo wa kununua mazao ya wakulima kwa wingi zaidi.
Kuhusu Kuwezesha Upatikanaji wa Mikopo kwa Vijana na Wanawake (BBT Mitaji) amesema Wizara kupitia Mfuko wa Dhamana wa Pembejeo za Kilimo (AGITF) itawezesha upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu ya Sh Bilioni tano kwa vijana na wanawake.
Vilevile,amesema Wizara itaweka kiasi cha Dola za Marekani Milioni 35 kwenye Benki za biashara kwa ajili ya guarantee scheme zitakazowezesha vijana na wanawake kupata 186 mikopo yenye riba nafuu mara mbili au zaidi ya fedha hizo. 5.2.4
Aidha Kuhusu Kuwezesha Vijana na Wanawake Kuongeza Thamani ya Mazao amesema Wizara kupitia Bodi ya Mkonge itaendelea kutoa mafunzo ya kuongeza thamani ya zao la mkonge kwa vijana na wanawake 200 ili waweze kuzalisha bidhaa zitokanazo na zao hilo.
;

