MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanawake Taasisi za Kitafiti Watoa Furaha Kwa Waliojifungua, Madaktari, Manesi Kawe Kituo Cha Afya
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanawake Taasisi za Kitafiti Watoa Furaha Kwa Waliojifungua, Madaktari, Manesi Kawe Kituo Cha Afya
Habari

Wanawake Taasisi za Kitafiti Watoa Furaha Kwa Waliojifungua, Madaktari, Manesi Kawe Kituo Cha Afya

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WANAWAKE wa Umoja wa Taasisi za Kimataifa za Utafiti (CGIAR), wakiongozwa na Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo cha Kitropiki (IITA), wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wanawake waliojifungua, madaktari na manesi katika Kituo cha Afya Kawe.

Taasisi nyingine zilizoshiriki ni Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo (ILRI), Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mpunga (IRRI) na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti na Ubunifu katika mnyororo wa thamani ya uvuvi (WorldFish)

Ofisa Mawasiliano wa IITA, Gloriana  Ndibalema amesema kwamba wanawake wa umoja huo ambao wanafanya utafiti wa kilimo wameamua kutoa msaada huo kutokana na michango waliyoichanga katika sekta ya afya kwenye wodi ya wazazi ya Kituo cha Afya Kawe ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

“Tunafanya utafiti wa kilimo nchi za kiafrika, katika Afrika Mashariki tunafanya utafiti Kenya, Tanzania, Uganda, Madagasca, Comoro.

“Tunafanya utafiti wa mihogo mahindi soya, jamii ya mbaazi, ndizi. Utafiti wetu tunaanzia maabara mpaka mnyororo mzima wa thamani,” amesema.

Amesema wameweza kutoa kompyuta mbili kwa ajili ya kituo hicho cha afya, vipimo vya mapigo ya moyo wa mtoto, mapazia, mipira wanayotumia wanawake wakijifungua, vitenge kwa ajili ya wazazi na madaktari na wauguzi, pamoja na vitambaa vya suruali kwa ajili ya watumishi wa wodi hiyo.

Vile vile wametoa mabeseni yaliyowekwa vifaa mbalimbali kwa ajili ya mtoto na mama kwa wazazi waliojifungua, walioruhusiwa kwenda nyumbani, walioko hospitalini na wanaotarajiwa kujifungua.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho cha Afya, Dkt. Isack Mbalwa ameshukuru kwa msaada huo uliotolewa na umoja huo wa wanawake, kwa kusema kuwa wanawake ni nguzo muhimu.

“Kwa zawadi hii mmewagusa na kuwafariji wamama hawa,” amesema.

Pia amesema kituo hicho kinatoa huduma mbalimbali, mwanzo kilikuwa ni zahanati lakini baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuongeza fedha waliongeza maabara, jengo la wama na jengo la kulaza wagonjwa.

“Kituo hiki kinatoa huduma ya kinywa na meno, wagonjwa wanaohudumiwa na kurudi nyumbani, matunzo kwa wenye ukimwi, kujifungua mama na mtoto pamoja na upasuaji,” amesema.

Naye muuguzi katika wodi hiyo ya wazazi Aisha Said ameshukuru wanawake hao kwa msaada walioutoa kwani ni wachache wenye moyo huo, wapo walio na uwezo lakini hawatoi msaada kama huo.

Mzazi Mar Mfikwa naye alishukuru umoja huo kwa upendo waliouonyesha kwao wazazi kwa kuwapatia mabeseni ya kuogeshea watoto pamoja na vifaa vingine mbalimbali.

You Might Also Like

Waziri Mkuu Majaliwa Akoshwa Na Tafiti Ya Mhitimu OUT

Dkt. Ndumbaro : Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Imefanikiwa 

Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88

Sera mpya ya biashara irahisishe ufanyaji biashara

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi
Next Article ALAT Kujadili Ripoti Ya CAG
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?