MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua
Habari

Vita Mashariki ya Kati Vyatikisa Uchumi wa SADC, Mawaziri Watakiwa Kuchukua Hatua

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Ronald Lamola, amesema kuwa hali ya sasa ya siasa za dunia pamoja na vita vinavyoendelea katika Mashariki ya Kati imesababisha madhara makubwa kimataifa, ikiwemo kwa nchi za SADC.
Lamola pia ni Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, amesema hayo wakati akifungua mkutano wa 47 wa Baraza hilo unaofanyika jijini Pretoria, Afrika Kusini Machi 12 na 13, 2026.
Habari Picha 11446
Amesema hali hiyo ni ujumbe muhimu kwa nchi za ukanda huo kuchukua hatua madhubuti za pamoja ili kujinasua na athari hizo.
Akizungumza katika mkutano huo, Lamola amesema kuwa mivutano ya kisiasa na vita vinavyoendelea vinatishia uthabiti wa mnyororo wa biashara duniani.
Habari Picha 11447
Ameeleza kuwa kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la kimataifa kutaongeza gharama za uzalishaji wa mbolea, hali ambayo inaweza kusababisha kupanda kwa bei za vyakula.
Kwa mujibu wa Lamola, hali hiyo ni tishio kubwa kwa usalama wa chakula katika ukanda wa SADC, hasa ikizingatiwa kuwa takribani watu milioni 58 tayari wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa chakula.
Habari Picha 11448
Aidha, ameeleza kuwa kutokana na hali ya vita katika Mashariki ya Kati, kuna uwezekano mkubwa kwa baadhi ya nchi za eneo hilo kupunguza au kusitisha mipango yao ya uwekezaji nje ya nchi na badala yake kuelekeza rasilimali katika masuala ya usalama wa ndani.
Ameonya kuwa hali hiyo inaweza kuwa na athari kubwa kwa ukanda wa SADC, hususan katika sekta za miundombinu, fedha, teknolojia, madini na nishati ambazo baadhi yake hutekelezwa kwa ushirikiano na nchi za Mashariki ya Kati.
Lamola pia amebainisha kuwa migogoro hiyo inaweza kupunguza juhudi za viongozi wa Afrika katika kutafuta suluhisho la tatizo la madeni kupitia majukwaa ya kimataifa.
Habari Picha 11443
Amesema kwa sasa nchi nyingi za Afrika hutumia fedha nyingi kulipa madeni, kiasi ambacho katika baadhi ya nchi huzidi hata bajeti za sekta za elimu na afya.
Kutokana na hali hiyo, amewataka mawaziri wanaoshiriki mkutano huo kutumia fursa hiyo kupanga mikakati madhubuti ya kukuza uchumi wa ukanda wa SADC, ambao bado unaendelea kukabiliana na athari za janga la COVID-19 pamoja na vita kati ya Urusi na Ukraine.
Habari Picha 11449
Katika mkutano huo, ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Maghembe, akifuatana na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula.

You Might Also Like

Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa

VETA yawafikia madereva ‘Boda boda’

Nyamhokya Atoa Wito kwa Wanawake Kusimama Imara Kiuchumi

TEA Yatathmini Utekelezaji na Kupanga Mwelekeo Mpya Kupitia Baraza la Wafanyakazi

Chinyeli Aahidi Chakula Bure kwa Wazee, Mwanyemba Kupambana Kutafuta Maendeleo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mamlaka Za Mitaa Ondoeni Urasimu Katika Kuanzisha Biashara Mpya-Waziri Mkuu
Next Article Tanzania, Afrika Kusini Zakubaliana Kuharakisha Makubaliano ya Ushirikiano
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yafikia Trilioni 11.2, Hifadhi Skimu Yatajwa Kubadili Maisha ya Watanzania
Habari April 27, 2026
TUCTA: Waajiri Watekeeze Nyongeza Ya Kima cha Mishahara Sekta Binafsi
Habari April 27, 2026
Serikali Yaweka Mkazo Kufufua Viwanda Musoma Ili Kuongeza Ajira
Habari April 24, 2026
Program Ya Mama Samia Ya Kurasimisha Ujuzi Yazinduliwa
Habari April 23, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?