Na Lucy Lyatuu, Dodoma
MAMLAKA Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi Stadi (VETA), kupitia kampuni tanzu ya ujuzi ya kuendeleza ujuzi imezalisha jumla ya bidhaa 825 za ubunifu ambazo zimekuwa zikiuzwa katika soko la ndani na nje ya nchi.
Meneja Ujuziwa Kampuni hiyo, katika Mamlaka hiyo, Marco Kapinga amesema hayo wakati akizungumza katika banda la VETA lililoko katika wiki ya utumishi wa Umma ,inayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park mkoani humo.

Kuhusu kampuni hiyo alisema inaendeleza uzalishaji na kuingia kwenye biashara katika bidhaa za samani,ngozi,asali na hata mafuta ya mgando na lengo likiwa ni kuongeza uwezo ambapo Mamlaka imefanikiwa kwa kiwango kikubwa.
Amesema katika bidhaa hizo zilizozalishwa zimetumia ubunifu na kuongeza uzalishaji na ujuzi ambapo katika bidhaa hizo 825 nyingi ni za maofisini, nyumbani na katika hoteli mbalimbali zilizoko Zanzibar.
“Nje ya n hi tumeuza bidhaa katika soko la Canada na sasa tuko kwenye kuandaa mkataba wa makubaliano na utakapokamilika tutausaini lakini pia katika soko la Urusi, hii ikiwa ni baada ya ziara ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan aliyoifanya hivi karibuni,” amesema Kapinga.
Kwa upande wake Meneja Rasilimali Watu wa VETA, Elihaika Manyanga amesema VETA imekuwa ikitumia wiki ya utumishi wa umma kueleza na kuonesha huduma mbalimbalimwanazotoa pamoja na kueleza mitaala itolewayo katika Mamlaka hiyo.

“Wanaotaka kujiunga na Mamlaka hii tunatumia wiki hii kuwakumbusha kuwa Julai ndio muda muafaka,na kwamba wanaweza kutumia mifumo mbalimbali ya mamlaka hiyo ili kujiunga,” amesema.


