MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yawasilisha Teknolojia ya Hybrid Katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yawasilisha Teknolojia ya Hybrid Katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana
Habari

VETA Yawasilisha Teknolojia ya Hybrid Katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: CHUO cha Ufundi Stadi (VETA) Mbeya kiimeonyesha teknolojia ya kisasa ya mfumo wa Hybrid kwa magari katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana yalnayoendelea mkoani humo.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mwanafunzi Adam Akyoo amesema teknolojia hiyo, inayowezesha gari kuendelea kuendeshwa kwa kutumia umeme hata mafuta yanapokwisha, inalenga kupunguza gharama za uendeshaji wa magari na kutoa suluhisho la muda mfupi kwa wamiliki wa magari ya kisasa yanayotumia nishati mchanganyiko.
“Tumewasilisha mfumo huu kama sehemu ya mafunzo tunayotoa kwa vijana wetu ili waendane na mabadiliko ya teknolojia, hasa kwenye sekta ya usafiri ambayo sasa inategemea magari ya umeme,” amesema.
Amesena mfumo huo wa Hybrid unaunganisha mota ya umeme kwenye injini ya gari, ambapo umeme huzalishwa na kusaidia kuendesha gari hata mafuta yanapokosekana. Hii husaidia kupunguza utegemezi mkubwa wa mafuta, hasa maeneo ya mbali ambapo vituo vya mafuta ni vichache.
“Kuna ongezeko kubwa la magari ya umeme nchini, lakini mafundi wengi hawana ujuzi wa kuyashughulikia. Hii ni fursa kwa vijana kujifunza na kuwa sehemu ya suluhisho,” amesena..
Habari Picha 9885
Kwa upande wake Ofisa Habari na Uhusiano wa VETA Taifa, David Mpondyo, amesema VETA kwa sasa imeongeza nguvu katika kufundisha fani zinazohusiana na teknolojia mpya, ili kuhakikisha vijana wa Kitanzania wanakuwa na ujuzi unaohitajika katika soko la sasa na la baadaye.
“Zamani tulikuwa tunafundisha zaidi magari ya dizeli na petroli, lakini sasa tunajikita kwenye magari ya umeme kwa kuwa ndiko dunia inaelekea. Tunataka vijana wetu wasipitwe,” amesema Mpondyo.
Amesema Kwa sasa, VETA ina zaidi ya vyuo 80 nchini, huku serikali ikitekeleza mpango wa ujenzi wa vyuo 65 vipya katika kila wilaya. Lengo ni kuongeza fursa kwa vijana wengi zaidi kupata mafunzo ya ufundi stadi kwa gharama nafuu, na kujiajiri au kuajiri wengine.
Amesema Katika baadhi ya vyuo kama VETA Dodoma na VETA Moshi, tayari kozi za kisasa kama uuzaji, ukarabati wa magari ya umeme, na welding ya viwango vya kimataifa zimeanzishwa ili kukidhi mahitaji ya miradi mikubwa kama vile bomba la mafuta la Afrika Mashariki (EACOP).
Mpondyo amehimiza vijana kuchangamkia fursa zinazotolewa na VETA kwa kuwa ndizo msingi wa ajira na maendeleo ya kiuchumi kwa mtu binafsi na taifa kwa ujumla.
“Kama hujaweza kufika chuoni, fika kwenye maonesho haya. Hapa utajionea kazi za mikono ya vijana wenzako na kujua namna ya kujiunga. Elimu ya ufundi si suluhisho la waliokosa, bali ni msingi wa maisha ya kisasa,” amesema.

You Might Also Like

Ruto: Diplomasia Itumike Kumaliza Mgogoro Kongo

Wapongeza Nyongeza Ya Likizo Kwa Aliyejifungua Mtoto Njiti

TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga

VETA Yatembelea Kiwanda Cha Kutengeneza Nyumba Bila Kutumia Tofali

Tume Ya Kurekebisha Sheria Tanzania Kuipitia Sheria Ya Takwimu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu
Next Article CHAUMMA Kuja Na Mpango Wa Masoko Ya Kisasa Dar es Salaam
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?