MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari

Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kuendeleza juhudi za kukuza mafunzo ya amali na stadi za kazi kwa kuhakikisha kunafanyika ufuatiliaji wa karibu katika vyuo vyote vinavyotoa taaluma hiyo, iwe ni vya umma au binafsi.

Vyuo hivyo ni pamoja na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii (FDC), na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Majaliwa ameagiza hayo wakati akifungua kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Habari Picha 9156

Amesema kuwa elimu ya ufundi stadi ni njia muhimu ya kuwawezesha Watanzania kupata maarifa na ujuzi utakaowasaidia kujipatia kipato, kujiajiri au kuajiriwa, hivyo kuchangia katika kukuza uchumi wa nchi.

“Tunataka kuongeza ujuzi wa Watanzania. Elimu ya ufundi stadi inapaswa kutolewa kwa kila mtu mwenye nia ya kujifunza, bila kujali kiwango chake cha elimu. Unaweza kuwa na shahada ya chuo kikuu lakini bado ukahitaji ujuzi wa ufundi,” amesema.

Amesisitiza ni lazima wanaohitaji kuwa mafundi katika fani mbalimbali, kama vile umeme, waende kusomea katika vyuo vinavyotoa elimu hiyo kwa vitendo.

Habari Picha 9157

“Logic bado iko pale pale kama unataka kuwa fundi umeme, lazima uende kwenye chuo kinachofundisha umeme,” amesema.

Pia amehimiza Wizara ya Elimu kuendelea na juhudi za kuhakikisha vyuo vya FDC na VETA vinaboreshwa na vinatoa elimu bora ya ufundi kwa wote.

Amesisitiza elimu hiyo iwe na mwelekeo wa kuwajengea Watanzania uwezo wa kuchangia kikamilifu maendeleo ya kiuchumi kupitia ujuzi wao.

“Lengo letu ni kuwawezesha Watanzania kupitia elimu ya watu wazima na stadi za kazi ili wajikwamue kiuchumi na kuleta mchango chanya kwa taifa,” amesema Waziri Mkuu.

Ametoa wito kwa taasisi zote zinazotoa mafunzo ya ufundi kushirikiana na serikali katika kuhakikisha elimu hiyo inafikia kila Mtanzania mwenye nia ya kujifunza na kuleta mabadiliko katika jamii.

You Might Also Like

TUCTA: Wafanyakazi Jitokezeni  Kwa Wingi Kwenda Kupiga Kura Mchague Viongozi Watakaolinda  Maslahi Yenu  

Rais Samia afurahia SGR

Gridi Ya Taifa Ni Dhaifu Kwa Mikoa Ya Kaskazini-Mramba

Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu

Muswada kuja wa Watumishi Wanaofanya Kazi Eneo Zaidi ya Moja Kuanza kuchangiwa na Waajiri Wote

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Next Article Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ubunifu Wa Majengo Watakiwa Kuzingatia Tija Na Gharama Nafuu
Habari April 11, 2026
Waziri Ulega aridhishwa na miradi ya dharura TANROADS
Habari April 11, 2026
Mbunge Majule ataka wanawake wapewe elimu ya fedha na mitaji
Habari April 11, 2026
Mbunge Msita Ataka Ukarabati Wa Haraka Barabara Zilizoharibiwa Na Mvua
Habari April 11, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?