MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Habari

Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
TAASISI  ya Wakala wa Barabara (TANROADS) na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) zimeagizwa kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja na  kumsimamia Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato ili mradi huo ukamilike kwa wakati na ubora.
Maelezo hayo yametolewa na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega wakati wa ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika Jiji la Dodoma.
Ulega ameelekeza Taasisi hizo kuwa na mawasiliano na ushirikiano wa karibu kwani Watanzania wanasubiria mradi huo na kuahidi kuukagua mradi huo mara kwa mara.
Ulega amesema mradi huo uliofikia  asilimia 53.9 ukikamilika utainua uchumi wa Mkoa wa Dodoma na kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji.
“Nimekagua jengo hili la abiria ambalo ni la kisasa na Mkandarasi yupo nyuma ya muda, hivyo nimeagiza Mkandarasi  Beijing Construction Engineering Group na Hebei Construction Group Corporation (BCEG) afanye kazi usiku na mchana na kuongeza idadi ya wafanyakazi,”  amesema Ulega.
Ameongeza kuwa Serikali haitaongeza muda kwa Mkandarasi huyo kama atashindwa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo kwa wakati na atapaswa kuilipa  Serikali fidia kwa kuchelewesha mradi.
“Nimetoa maelekezo kwa miradi yote Makandarasi wanapochelewesha miradi ambayo tuna uhakika tunayo fedha lazima tuwadai fidia,” amesema.
Waziri Ulega ameridhishwa na hatua za ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato ambayo imefikia asilimia 89 na kupongeza TANROADS na Mkandarasi Sinohydro kwa hatua hiyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuufungua mkoa huo kwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa kiwanja hicho ambapo amesema uwepo wake ni fursa ya kijamii na kiuchumi kwa wana Dodoma na nchi kwa ujumla.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Abdul Mombokaleo amesema wanatarajia kuanza majaribio ya kuruhusu urukaji na utuaji wa ndege katika kiwanja hicho ifikapo mwezi Juni, 2025.

You Might Also Like

JAB Yatoa Mwezi Moja Kuthibitishwa, kupewa vitabulisho

Homa ya nyani mjadala wa dharura kwa mawaziri wa afya Afrika

Serikali Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini

TEA, UNICEF na Canada waendeleza mageuzi ya elimu Sikonge

Thamani ya Fedha Ionekane Kwenye Utekelezaji wa Miradi-Nyamoga

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee
Next Article Hali Ya Ulinzi Na Usalama Wa Mipaka Ni Salama
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Kijaji: Huduma ya Kudungwa na Nyuki Kuongeza Kinga Yavutia Bungeni
Habari May 15, 2026
Serikali  Kutumia Fursa  ya AFCON,  Miss World Na IPU Kukuza Utalii Nchini
Habari May 15, 2026
TFS Yavunja Rekodi Utalii Wa Misitu,Mapato Yapaa Kwa Asilimia 43
Habari May 15, 2026
Serikali Kuimarisha Uvuvi Bahari Kuu Kupitia TAFICO
Habari May 14, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?