MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tume ya umwagiliaji yapambana kuinua kilimo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tume ya umwagiliaji yapambana kuinua kilimo
Habari

Tume ya umwagiliaji yapambana kuinua kilimo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi

DODOMA: MWAMKO wa ulipaji tozo kwa wakulima wanaotumia skimu za umwagiliaji katika maeneo tofauti nchini, umewezesha Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kupata sh bilioni mbili kwa mwaka 2024, ambazo zinaendeleza ujenzi mwingine.
Ofisa Kilimo Mwandamizi kutoka Tume ya Umwagiliaji, Lukombeso  Udumbe ameeleza hayo katika maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi yanayoendelea jijini Dodoma.
Amesema Sheria ya Tume ya Mwaka 2013, namba nne, imeipa tume jukumu la kuhakikisha wakulima wakianza kuzalisha wanatoa tozo katika skimu ambazo uwekezaji umefanywa.
Amesema eneo hilo wamefanikiwa kulisimamia na kuwawezesha kupata kiasi hicho cha sh bilioni mbili kutoka sh milioni 150 kwa mwaka 2021/ 2023.
Amesema mbali na tozo hiyo, nusu ya bajeti ya Wizara ya Kilimo kuanzia mwaka 2022/2023 na 2023/24  ilikwenda kwenye tume hiyo kwa ajili ya skimu za umwagiliaji.
 Akizungumzia tozo hiyo ya wakulima, anaeleza kuwa kiasi kinachokusanywa kinaendeleza ujenzi wa miradi mingine  ili sekta ya umwagiliaji iwe endelevu.
“Na hadi sasa tumeweza kuongeza eneo kubwa la umwagiliaji ukilinganisha na miaka ya nyuma. Kazi kubwa imefanyika ikiwa ni pamoja na kujenga mabwawa makubwa, lengo likiwa ni kuvuna maji ambayo yalikuwa yanapotea kwa kiasi kikubwa sana,” amesema.
Amesema kazi ya tume hiyo ni kuendeleza kilimo cha umwagiliaji kwa kuangalia maeneo ya wakulima na kuyafanyia tathmini kuangalia eneo husika kama linafaa.

You Might Also Like

Mfumo wa Usalama Majumbani, Umewakumbuka Wenye Ulemavu

UTT AMIS Yazindua kampeni ya ‘Kijiwe Mchongo

SADC Yabaini Changamoto Kuu katika Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Kikanda

Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma

Serikali Kulinda Wabunifu Wa Silaha

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Someeni fani zisizo maarufu – mwalimu
Next Article TASAC yajipanga kuhudumia wafanyabiashara
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Sheria Ya  Kuzuia Shisha Kutungwa, Yabainika Kuwekwa Dawa Za Kulevya
Habari May 29, 2026
Waraibu Wa Dawa Za Kulevya 85,425  Wapatiwa Huduma Ya Tiba Nchini Kwa Mwaka 2025
Habari May 29, 2026
NHC Kuendelea Kutekeleza Miradi Mikubwa Ya Kimkakati Ya Ujenzi Wa Nyumba
Habari May 28, 2026
Kutokulipa Kodi Ya Pango La Ardhi Unakosa Sifa Za Kugombea Nafasi Za Uongozi
Habari May 28, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?