MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Sheria Ya Kupata  Taarifa, Ya NGOs Zina Upungufu 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Sheria Ya Kupata  Taarifa, Ya NGOs Zina Upungufu 
Habari

Sheria Ya Kupata  Taarifa, Ya NGOs Zina Upungufu 

Author
By Author
Share
6 Min Read
Mwandishi wetu
ARUSHA: TAASISI zisizo za kiserikali nchini zimeiomba Serikali ya Tanzania  kuzifanyia maboresho sheria  ya Kupata taarifa ya mwaka 2016 na sheria ya mashirika yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002 ili kuondoa upungufu uliopo.
Meneja uchechemuzi  wa Kituo cha sheria na haki za Binaadamu nchini(LHRC), Wakili Raymond Kanegene.akizungumza katika kikao kazi
cha kupitia sheria hizo ambacho kiliwashirikisha wadau kutoka serikalini na sekta binafsi amesema sheria hizo zinahitaji maboresho madogo ili ziwe bora zaidi.
Wakili Kanegene amesema kwa mujibu wa maoni ya wadau na utafiti uliofanywa na Taasisi ya kimataifa ya CIPESA unaonesha kuwa,katika ukanda wa nchi za Afrika  ya Mashariki licha ya kila nchi kuwa na sheria zake ikiwepo sheria ya kupata taarifa     lakini imebainika kila nchi sheria hiyo ina mapungufu. yake.
Amesema kwa mfano sheria ya kupata taarifa  ya Tanzania  kifungu cha  5(1) kinatoa haki za kila mtu kupata  taarifa    lakini  5(4) kinasema ambao wanaweza kupata taarifa lazima wawe raia wa Tanzania.
“kifungu kama hiki kinapaswa kitowe haki ya kila mtu kupata  taarifa lakini kinaweza kuziweka taarifa katika makundi ni zipi anapaswa kupewa raia tu na taarifa zipi hapaswi kupewa mtu ambaye sio raia,” amesema.
Kanegene amesema uchambuzi wa sheria hiyo ya kupata taarifa kifungu cha  9 kinaeleza mtu ambaye anataomba     taarifa atapewa taarifa hiyo sio zaidi ya siku 30 .
Amesema muda huo ni  mrefu  tofauti na sheria za nchi nyingine za Afrika Mashariki, ambapo Rwanda utapewa taarifa ndani ya siku 3 ,Kenya siku 21, Uganda siku 21 na Sudan Kusini siku 7.
“Mapendekezo ya wadau siku ziwe chache kwani mwandishi wa habari hawezi kusubiri kupata taarifa ndani ya siku 30 kwani taarifa inapaswa kutolewa kwa wakati,” amesema..
Akichambua sheria ya NGOs  amesema pia ina upungufu ambao unaathiri sekta hiyo, miongoni mwa upungufu huo ni kutaka kila baada ya miaka  10 NGOS kupata usajili mpya, kuwepo sheria kali za  kuzifunga ikiwepo kwa kushindwa kuwasilisha tu taarifa kwa taasisi zaidi ya tatu.
“lakini pia sheria hii imekuwa ikitaka kuwasilisha mikataba ya wahisani kabla ya kupata ufadhili lakini pia kutangaza kwenye vyombo vya habari taasisi inapopata zaidi ya sh 20 milioni  mambo ambayo yanahitai maboresho”amesema
Amesema mapendekezo ni kuondolewa kifungu ambacho kinataka NGOs kusajiliwa upya kila baada ya miaka 10 ,kuwa na mfumo mmoja kutoa taarifa za utendaji  na fedha wa NGOs ili taasisi zote ziweze kupata  lakini pia kuwekwa utaratibu rafiki kutangaza miradi na mikataba yake.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya habari nchini(JOWUTA) Mussa Juma alisema  maboresho ya sheria hizo yataongeza weledi katika.kufanya kazi na kuondoa migogoro isiyo ya lazima.                                         Alisema sheria ya kupata taarifa bado haijatumika vizuri na wadau wengi hawaijuwi lakini ingekuwa nzuri ingesaidia sana kuondoa kuandokwa habari ambazo sio sahihi.                 ” kunapokuwa na urasimu.wa kupata taarifa ndipo taarifa potofu usambazwa hivyo ni muhimu kuwa na sheria rafiki kwa wadau”alisema
Mwenyekiti wa Taasisi ya habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA -TAN) Edwin Soko  akichangia mjadala huo, alisema ni muhimu sheria kadhaa kuboreshwa kwendana na matakwa ya Katiba ya nchi na mikataba ya kimataifa.
“kuna  taarifa nyeti ambazo kutolewa lazima kuwepo na utaratibu ikiwepo taarifa za masuala ya ulinzi na usalama na jambo hili hata katika maadili ya uandishi wa habari linajulikana”alisema
Amesema sheria ya kupata taarifa inaathiri wanahabari kwani l kwa mwandishi wa habari kuambiwa asubiri ndani ya siku 30 kupata taarifa ambayo anahitaji  ni muda mrefu.
Mwenyekiti wa Kikosi kazi hicho, Sophia Komba akizungumza katika kikao hicho, alisema sheria nzuri ni zile ambazo zinasaidia ukuaji wa sekta husika na sio ambazo zinaathiri sekta husika.
Amesema sheria ya NGOs inahitaji maboresho makubwa ili kwendana na maoni ya wadau kwani sasa imekuwa ni tishio kwa sekta hiyo na kuanza kuathiri uendelevu wa mashirika  mengi yasiyo ya kiserikali.
Ofisa Utetezi wa Mtandao wa Mashirika ya Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini(THRDC) Paul Kisabo alisema sheria ya kupata taaria na sheria ya NGOs ni baadhi tu ya sheria ambazo zinahitaji maboresho kwa baadhi ya vifungu.
Wakili Kisabo amesema, binafsi amewahi kutumia sheria hiyo, kuomba taarifa katika taasisi ya Umma  lakini kwa zaidi ya miezi sita sasa hajapata licha ya kufanya jitihada kubwa na hilo linawezekana kutokana na mapunguu ya sheria hiyo ya kupata taarifa.
Akifunga kikao hicho,Komba alitaka wadau walioshiriki kuendelea na majadiliano lakini pia kuongeza taasisi nyingine za serikali katika vikao vijavyo ili kuwa na uelewa wa pamoja wa sheria hizo na kujua mapungufu yake.
Kikao kazi hicho, kilichoandaliwa na LHRC ,kilishirikisha  maofisa kutoka  Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo,Tume ya kurekebisha sheria, Chama.cha Mawakili.wa Tanganyika(TLS), Jumuiya ya kikristo Tanzania(CCT ) ,
Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania(JOWUTA), MISA- TAN, maofisa kutoka Wizara ya Sheria na Katiba,  Wizara ya Maendeleio ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum,Baraza la Habari  Tanzania(MCT) Jukwaa la wahariri(TEF) ,Jamii Afrika, na Mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali nchini.

You Might Also Like

TFRA yazindua Chama cha wafanyabiashara wa Mbolea

Polisi Yaimarisha Usalama Timu za Simba na Yanga Kesho

Jeshi la Uhifadhi watakiwa kuzingatia mafunzo – Wakulyamba

Matumizi Holela Ya Vilevi Hatari Kwa Watumiaji

China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mchengerwa Awafunda Walimu
Next Article Viongozi Bora Hujenga Mazingira Wezeshi Kwa Wahadhiri – Profesa Nombo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?